Azam wakishangilia bao
Kwa mantiki hiyo, Azam, mechi yao ya mwisho dhidi ya Mgambo itakuwa ni kuweka heshima tu na ilihali kwa Simba, haitakuwa na maana hata akishinda mechi yake ya mwisho.
Simba haitaweza tena kuifikia Azam, ambayo kwa ushindi wao dhidi ya Yanga, wamefikisha pointi 48, wakati Simba, hata akishinda mechi yake iliyobaki dhidi ya JKT Ruvu itafikisha pointi 47.
Ushindi huo, unaifanya Azam FC ifikishe pointi 48 baada ya kucheza mechi 25, nyuma ya mabingwa, Yanga SC wenye pointi 55 za mechi 25.
Yanga, kwa kuwa mabingwa, wataiwakilisha Tanzania Bara katika Kombe la Washindi Afrika mwakani wakati Azam itashiriki kombe la Shirikisho na kuifanya Simba, moja ya klabu kongwe, kuwa nje ya mashindano ya kimataifa kwa zaidi ya miaka 3 mfululizo
Baada ya mechi hiyo, Yanga ilikabidhiwa kombe hilo mbele ya mashabiki, ambao hawakujali kipigo cha timu yao na kuwa kwa kuwa na furaha ya ubingwa
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.