0
Antoine GriezmannHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Mshambuliaji Mfaransa anayechezea Atletico Madrid Antoine Griezmann anataka kujua hatima yake katika klabu hiyo kabla ya kusafiri kwenda kucheza Kombe la Ufaransa. Mchezaji huyo wa miaka 27 amehusishwa na kuhamia Barcelona. (L'Equipe kupitia Sky Sports)
Tottenham nao wanakusudia kutumia kifungu cha £3m kumfungua Jonny Evans kutoka kwa mkataba wake West Brom iwapo timu hiyo itashushwa daraja. Mchezaji huyo wa miaka 30 kutoka Ireland Kaskazini huenda pia akatafutwa na Arsenal. (Telegraph)
Juventus wamesitisha juhudi zao za kumtafuta beki kamili wa Uhispania anayechezea Arsenal Hector Bellerin, 23. Hii ni kwa sababu wana imani kwamba watafanikiwa kumchukua beki Mwitaliano Matteo Darmian, 28, kutoka kwa Manchester United. (Goal)
Hector BellerinHaki miliki ya pichaEPA
Image captionHector Bellerin
Mshambuliaji wa Arsenal Lucas Perez, 29, anataka kurejea katika klabu hiyo ya Ligi ya Premia baada ya kutofanya vyema akiwa kwa mkopo Deportivo La Coruna. Mhispania huyo alizomewa na mashabiki majuzi baada yake kuendelea kutofanya vyema. (Independent)
Kipa wa Atletico Madrid na Slovenia Jan Oblak amesema hana uhakika iwapo atasalia katika klabu hiyo msimu ujao. Arsenal wanataka sana mlindalango huyo wa miaka 25 ajiunge nao kuchukua nafasi ya Petr Cech, 35, atakapostaafu. (London Evening Standard)
Jan OblakHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionJan Oblak alitia saini mkataba wa miaka sita Atletico Madrid mwaka 2014
Kipa wa Chelsea kutoka Argentina Willy Caballero, 36, atasalia katika klabu hiyo hadi Juni 2019. Hata hivyo, kipa wao nambari wani Thibaut Courtois, 25, bado anaweza kuihama klabu hiyo. Courtois mkataba wake utafikia kikomo mwisho wa msimu. (Goal)
Kiungo wa kati wa zamani wa Italia Andrea Pirlo huenda akapewa kazi yake ya kwanza kabisa ya ukufunzi katika timu ya taifa iwapo mmoja kati ya Carlo Ancelotti na Antonio Conte ndiye atapewa kazi ya kuwa meneja wa timu ya taifa. (Gazzetta dello Sport kupitia Football Italia)
Paris St-Germain wanataka kocha wa Juventus Massimiliano Allegri ajiunge nao kumrithi Unai Emery mwisho wa msimu. (ESPN)
Usain BoltHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUsain Bolt alifanya mazoezi na Mamelodi Sundowns Januari
Bingwa wa Olimpiki mara nane Usain Bolt atafanya mazoezi na klabu ya Borussia Dortmund inayocheza Bundesliga katika kikao cha mazoezi ambacho kitakuwa wazi kwa umma. (Yahoo Sports)
Kiungo wa kati wa Bournemouth Lewis Cook, 21, atajishindia £17,000 kutoka kwa babu yake iwapo atateuliwa kuchezea England dhidi ya Uholanzi au Italia. (Yorkshire Evening Post)
Erik PietersHaki miliki ya pichaEMPICS
Image captionPieters ana mkataba wa kumuweka Stoke hadi 2020
Na beki wa Stoke mwenye miaka 29 Erik Pieters kutoka Uholanzi ameomba radhi baada yake kuvunja amri ya kutotoka nje kwenda kwa burudani katika kilabu kimoja kabla ya mechi ya Stoke na Everton wikendi iliyopita. (Stoke Sentinel)
Next
Haki miliki ya pichaIKULU, TANZANIA Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu (AfCHPR) imeamua kwamba Tanzania ilikiuka baadhi ya haki za wanamuziki Nguza Viking maarufu Babu Seya na mwanaye, Johnson Nguza 'Papii Kocha' katika kesi ambapo wawili hao walikuwa wamehukumiwa kufungwa jela maisha. Wawili hao waliwasilisha rufaa katika mahakama hiyo mwaka 2015 kupinga hukumu ya kifungo cha maisha iliyokuwa imetolewa dhidi yao. Majaji wa mahakama hiyo wamesema haki zao zilikiukwa kwa kutowapa taarifa za mashahidi wa upande wa mashtaka na kwamba mashahidi hao hawakuhojiwa mahakamani. "Mahakama inatambua kwamba taifa lililoshtakiwa halijapinga madai kwamba walalamishi hawakupewa taarifa za mashahidi na kwamba mashahidi wanne hawakuitwa kuhojiwa," majaji wamesema. Majaji hao wamesema kila mshtakiwa ana haki ya kupata muda wa kutosha na rasilimali za kutosha kujiandaa kujitetea. Aidha, kila mshtakiwa ana haki ya kuwahoji mashahidi waliowasilishwa dhidi yake. "Katika kesi hii, walalamishi wangepewa nakala za mashahidi wa mashtaka kuwawezesha kujiandaa kujitetea. Kwa hili kutofanyika, waliwekwa katika hali iliyowabana ukilinganisha na upande wa mashtaka, kinyume na kanuni ya usawa wa nguvu ya silaha. "Aidha, kwa kutowaita mashahidi hao wanne watoe ushahidi mahakamani, walinyimwa fursa ya kuwauliza maswali, na hili liliwaweka katika nafasi iliyowabana." Majaji walisema hilo lilikuwa ukiukaji wa Kifungu cha 7 (1c) cha Mkataba unaounda mahakama hiyo kwa upande wa serikali ya Tanzania. Hata hivyo, mahakama hiyo imesema madai ya wawili hao kwamba haki zao zilikiukwa wakati wa kutambuliwa hayana msingi. Aidha, mahakama haikupata ukiukaji wowote wa haki kwa kukataliwa kwa ushahidi wao kuhusu eneo walipokuwa wakati wa kutekelezwa kwa uhalifu huo. Kuhusu kwamba matokeo ya kupimwa mkojo na damu hayakuwasilishwa, mahakama hiyo imesema haki zao hazikukiukwa kwani matokeo hayo hayakutumiwa na Mahakama Kuu wala Mahakama ya Rufaa kuamua kwamba walikuwa na hatia. Hata hivyo, kuhusu ombi la mmoja wa washtakiwa apimwe uwezo wake wa kuzaa, mahakama hiyo imesema Tanzania ingefanikishwa apimwe. "Matokeo ya hilo yangebaini iwapo Bw Nguza angetekeleza uhalifu aliodaiwa kutekeleza. Mahakama inaamua kwamba kukataliwa kwa ombi hili, Tanzania ilikiuka haki zake kama zilivyoelezwa katika Kifungu 7 (1c) cha Mkataba unaounda Mahakama hii." Kupitwa na wakati Bw Nguza na mwanawe walikuwa pia wamedai jaji alikuwa anabagua lakini Mahakama hiyo imeamua hali kwamba baadhi ya washtakiwa walipatikana bila hatia na mashtaka yakapunguzwa, hiyo ni ishara kwamba kesi hizo ziliangaziwa kwa uzito wake. "Walalamishi hawajatoa ushahidi wa kutosha kuonesha jaji alikuwa na mapendeleo," majaji hao wameamua. Walalamishi walikuwa wameomba waachiliwe huru kwenye rufaa yao walipoiwasilisha mwaka 2015 lakini majaji wamesema hilo limepitwa na wakati kwani wawili hao waliachiliwa kupitia msamaha wa rais. Tanzania imetakiwa "kuchukua hatua zote ziwezekanavyo kurejesha haki za walalamishi." Walalamishi walikuwa wamewasilisha ombi la uamuzi kuhusu kulipwa fidia lakini majaji wamesema hakuna aliyewasilisha hoja kwa maandishi kuhusu ulipaji fidia. Walalamishi wametakiwa kuwasilisha hoja yao katika kipindi cha siku 40 nayo serikali ya Tanzania ijibu katika siku 40 baada ya kuwasilishwa kwa hoja hiyo. Bw Nguza na mwanaye walikuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa kuwabaka wasichana 10 wa shule waliokuwa na kati ya umri wa miaka 6 na 8 mwaka 2003 na walikuwa wametumikia kifungo cha miaka 13 kufikia wakati wa kupewa msamaha. Babu Seya ambaye ni miongoni mwa wafungwa 1,821 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya Uhuru wa Tanganyika mnamo 9 Desemba, 2017. Wengine 8,157 walipunguziwa adhabu zao. Wawili hao ndio walioimba kibao maarufu cha 'Seya' na walikuwa kati ya wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kufungwa maisha au kunyonga ambao walinufaika kutokana na msamaha wa rais. Wafungwa waliosamehewa wamshukuru Magufuli kwa kumwimbia Babu Seya na wanawe waachiwa huru kwa msamaha wa rais Hukumu katika kesi yao ilikuwa imepangiwa kusomwa Jumatano wiki hii lakini baadaye ikaahirishwa hadi leo. Hatua ya Dkt Magufuli kuwasamehea wawili hao ilishutumiwa na watetezi wa haki za watoto na wanawake. Kate McAlpine, mkurugenzi wa shirika la Community for Children Rights lenye makao yake Arusha aliambia BBC wakati huo kwamba alikuwa "ameshtushwa lakini hakushangazwa" na hatua ya rais huyo. Alisema hatua hiyo ilionesha 'uelewa mdogo' wa kiongozi huyo kuhusu masuala ya udhalilishaji wa watoto. Haki miliki ya pichaIKULU Image caption Nguza Viking na wanawe walipokutana na Magufuli Alilinganisha hatua hiyo na tamko la Rais Magufuli kwamba wasichana wanaoshika mimba hawafai kuwa shuleni. Matamshi ya Magufuli yawakasirisha wanawake Tanzania "Huwa hafahamu vyema mambo, hasa yanayohusu watoto kama waathiriwa. Wasichana wanaoenda shule hushika mimba kwa sababu mara nyingi ni waathiriwa wa udhalilishaji," alisema Bi McAlpine. Ilikuwaje hadi tukafika hapa? Nguza Viking na Johnson Nguza ni baba na mwanaye na ni raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao walikuwa wanamuziki Dar es Salaam. Wote walikamatwa 12 Oktoba, 2003 na kuzuiliwa kituo cha polisi cha Magomeni ambapo baadaye walifikishwa kizimbani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu 16 Oktoba, 2003 na kufunguliwa mashtaka 10 ya ubakaji na 11 ya ulawiti. Waathiriwa wao walikuwa watoto wa kati ya miaka sita na nane, na walikuwa wote kutoka darasa moja. Waathiriwa hao walidaiwa kubakwa na kulawitiwa kwa zamu na wanaume watano. Mnamo 25 Juni, 2004 hakimu aliwapata na hatia na kuwafunga jela Nguza na wanawe watatu. Mshtakiwa wa nne, ambaye alikuwa mwalimu, alipatikana bila hatia. Washtakiwa walikata rufaa Mahakama Kuu lakini rufaa yao ikatupwa. Walikata rufaa tena katika Mahakama ya Rufaa. Wawili kupatikana bila hatia Mwaka 2010 rufaa yao ilisikilizwa na 30 Oktoba Majaji Nathalia Kimaro, akisaidiana na Mbarouk Mbarouk na Salum Masati katika Mahakama ya Rufaa wakawaachilia huru Nguza Mashine na Francis Nguza baada ya kuwapata bila hatia. Babu Seya na mwanaye Papii Kocha walipatikana na hatia na hivyo kuendelea kutumikia adhabu ya kifungo cha maisha jela. Majaji walisema kuwa kuna uthibitisho kuwa warufani hao wawili waliwabaka watoto wa shule ya msingi mwaka 2003. Kesi hiyo iliwashtua mashabiki wa mwanamuziki Viking nchini Tanzania, na kanda nzima ya Afrika Mashariki. Mwanamuziki huyo mwenye kuimba nyimbo za rhumba, ambaye ni mzaliwa wa DRC, ameishi Tanzania kwa miaka mingi na kuwa na mashabiki wengi.
Previous
MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMAMOSI MACHI 24,2018

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top