Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameunga mkono
jitihada za kupambana na dawa za kulevya nchini kama hatua ya kuliokoa taifa na
janga hilo ambalo limesababisha madhara makubwa katika jamii.
Makamu wa
Rais ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na watendaji wa halmashauri ya wilaya
ya ILEMELA mkoani Mwanza.
Amesisitiza
kuwa mapambano dhidi ya dawa za kulevya yatakuwa ni endelevu lengo likiwa
kukomesha kabisa uuzaji, usambazaji na utumiaji wa dawa hizo kama hatua ya
kuokoa kizazi cha sasa na kijacho nchini.
Kuhusu
tatizo la uvuvi haramu, Makamu
wa Rais amewaagiza viongozi wa mikoa ya kanda ya Ziwa wakiwemo viongozi wa
Mwanza na mikoa mingine nchini kuanzisha mara moja oparesheni kali ya kupambana
na wavuvi haramu katika Ziwa Victoria ambao wamechangia kwa kiasi kikubwa
kupungua kwa samaki katika Ziwa hilo.
Wakati
huo huo halmashauri ya wilaya ya ILEMELA,
imetekeleza maagizo 14 yaliyotolewa na Makamu wa Rais aliyoyatoa mwaka
jana alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo likiwemo suala la watumishi wa
halmashauri kukaa karibu na maeneo ya ofisi ambapo mpaka sasa wakuu wa idara 23
wanaishi ndani ya wilaya ya ILEMELA ikilinganishwa na hapo awali ambapo
watumishi hao walikuwa wanakaa nje ya wilaya hiyo hali ambayo inatajwa
ilichangia kuzorotesha utendaji kazi kwenye halmashauri hiyo.
Kufutia
hali hiyo, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu
Hassan ambaye pia ni mlezi wa halmashauri hiyo amepongeza viongozi wa wilaya
hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri kwa kutekeleza maagiza yake kwa haraka
na kwa wakati.

Post a Comment