Jeshi la polisi
Zanzibar limeanzisha uchunguzi wa taarifa za utakatishaji wa fedha kwa watu
wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.
Kamishna wa polisi Zanzibar
Hamdan Omar Makame ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Bahari Fm ofisini
kwake Ziwani mjini Unguja, amesema uchunguzi huo wanaufanya kwa kushirikiana na
idara ya usalama wa taifa ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP na mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu wa
uchumi Zanzibar ZAECA na taasisi za fedha.
Amefahamisha kuwa,
wameanza uchunguzi kwa kuwahoji baadhi ya wanaotuhumiwa pamoja na kuchunguza
mfumo wao wa fedha ili kuwagundua wahusika na kuwachukulia hatua za kisheria.
Amefafanua kuwa, uchunguzi
huo pia utahusisha maduka ya kubadilishia fedha kutokana na tuhuma fedha nyingi
chafu zimekuwa zikipitishwa huko.
Aidha amesema njia hiyo
itasaidia kupata kwa kina taarifa na watakaogundulika majina yao yatatajwa
hadharani.

Post a Comment