Viongozi wa
vyama vya siasa
wametakiwa kushirikiana na
kuondoa chuki pamoja na fitna ili
kuleta maendeleo nchini.
Rai hiyo imekuja baada
ya wajumbe wa kikao cha halmashauri kuu ya CCM mkoa wa magharibi kichama kukutana
katika ukumbi wa
hoteli ya ngalawa iliyopo bububuu
kihinani kujadiliana masuala
mbaimbali juu ya
utendaji kazi kwa mwaka unaomalizika 2016 na unaoanza 2017.
Balozi Seif Ally Iddi makamo wa pili wa Raisi Zanziba na mlezi wa chama cha Mapinduzi Zanzibar
Akizungumza katika
kikao hicho mlezi wa chama cha mapinduzi CCM Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi
ambae pia ni makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar
amesema kuwa ni
vyema kuondoa chuki
katika utendaji wa
kazi na kukaa
kwa pamoja kufanya
kazi kwa umakini
ili kusogeza maendeleo
mbele.
Nae mkuu
wa mkoa mjini
magharibi Ayoub Mohammed
Mahmoud amesema kuwa
baadhi ya masheha
wamekuwa na tabia
ya kushiriki katika
kuuza viwanja katika
maeneo ya mabonde
hali ambayo ni
hatarishi kwa wananchi na kusema kuwa atakae kundulikana
kufanya hivyo hatua kali zitachukuliwa juu yake.
Post a Comment