Bodi ya chakula na vipodozi Zanzibar
imekanusha taarifa zilizoenea kuwa imethibitisha matumizi ya vipodozi aina ya
karolaiti kwa matumizi ya binadamu.
Akizungumza
na kituo kimoja cha redio visiwani Zanzibar , mkuu wa biashara na uwendeshaji
kutoka bodi hiyo Abdul-aziz Shaib amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote na
kusisitiza kuwa matumizi ya vipodozi hivyo ni hatari kwa matumizi ya afya ya
binadamu.
Aidha ametoa onyo kwa wafanyabiashara wanaoendelea kuuza bidhaa hiyo na kusema Serikali haitosita kuwachukulia hatua za kisheria kwa watakaobainika.
Pamoja na hayo Abdul-aziz ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kwenye mamlaka zinazohusika pindi wanapobaini duka linalouza vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku kwa matumizi ya binadamu.
Mkuu wa biashara na uwendeshaji
kutoka bodi ya chakula na vipodozi Zanzibar Abdul-Aziz Shaib akizungumza na
waandishi wa habari
Aidha ametoa onyo kwa wafanyabiashara wanaoendelea kuuza bidhaa hiyo na kusema Serikali haitosita kuwachukulia hatua za kisheria kwa watakaobainika.
Pamoja na hayo Abdul-aziz ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kwenye mamlaka zinazohusika pindi wanapobaini duka linalouza vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku kwa matumizi ya binadamu.
Post a Comment