0



MKUU  WA MKOA  LINDI  GODFRAY  ZAMBI  AKIZUNGUMZA NA  WAKAZI  WA KIJIJI  CHA  MAVUJI WILAYANI  KILWA  MKOANI LINDI
 
Wananchi  wa  kijiji  cha  Mavuji  wilaya  Kilwa  Mkoani Lindi  wameuomba  uongozi wa mkoa  huo  kusimamia  kurudishwa  kwa  maeneo  yao zaidi ya hekta  elfu 20 ziliyochukuliwa  na  wawekezaji  ambalo  halijafanyiwa  kazi ili kusudiwa.
 
Malalamiko  hayo  yametolewa  na  wananchi hao kwenye  mkutano wa hadhara  wa  mkuuu  wa mkoa  wa Lindi Godfrey  Zambi  ambaye  alikuwa moja ya  ziara yake wilaya  humo  kuhimiza  shughuli  za  maendeleo.
 
Akizungumza  kwa  niaba  ya  wananchi hao  Ali  Hemedi  alisema   mwaka  2008  shirika  la  bioshape  lili kiomba  kijiji   eneo  la  majaribio  ya  kupanda  miti ya  aina ya  mibono  baada ya kuwapa walishindwa kuendelea na mradi  kama  ilivyokusudiwa
Hemedi  alisema  kushindwa  kuendelea  kwa  mradi  huyo ambao ulichukua  hekta 16,000 umekifanya  kijiji  na wananchi  kukosa  eneo  la kuendesha shughuli za kilimo  na kuwafanya  kuwa  masikini  kwa  kupatwa  na  njaa  kila mwaka.
 
Sophia  Kilwanda  alisema sambamba  na  Mwekezaji   Bioshape  walitokea  Wawekezaji Alhashumu Company  Ltd  na Nitro Explossive  Ltd   wamechukua  hekta  zaidi  ya 6000 ambazo  wananchi  wenyewe  hawakushirikishwa  kikamilifu.
 
 Sophia  alisema kutokana  kutoshirikishwa wanamuomba  mkuu  wa  mkoa kuwasaidia  kwa hilo  hili  Haki  zao  waweze  kuzipata.
Yusuphu  Mohamedi alisema  migogoro ya ardhi  wilayani humo  inasababishwa  na watendaji  wa idara ya  ardhi inayoongozwa  na Hamidu Mtemekela   ambaye amekuwa  chanzo cha   matatizo  hayo. 
 
Kwa  upande  wake  mkuu  wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi  alisema  ofisi yake  italishughulikia  suala hilo  na aliwataka  watendaji   wa  halmashauri  ya wilaya  Kilwa  akiwemo afisa  Ardhi  kupeleka  vielelezo   vinavyo husu  migogoro  hiyo.
Zambi  alisema   wilaya  kilwa  inaongoza  kwa kuwa  na migogoro  ya  ardhi  katika  mkoa  wa  Lindi hali ambayo hailete  sura  mzuri  na ana amini kuwa  kuna  kasoro  za  kiutendaji  ambazo  zanahitaji  kurekebishwa.

Post a Comment

 
Top