0
                   Mkuu wa wilaya ya Liwale Mh Ephraim Mmbaga ambaye ndio mgeni rasmi



Shule ya sekondari ya Liwale high school imefanya mahafali ya wanafunzi 148 kidato cha nne mahali yaliyofanyika katika ukumbi wa Malecela uliopo shuleni hapo leo ambapo mgeni rasmi ni mkuu wa wilaya ya Liwale mheshimiwa Ephraim Mmbaga.

Liwale high school ilianzishwa mwaka 1990 na kuanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano mwaka 2008 na kuweza kufanyikiwa kufaulisha idadi kubwa ya wanafunzi na kuweza  kujiunga na vyuo mbalimbali.

Mkuu wa shule Elly John Moses hiyo akisoma risala mbele ya mgeni rasmi alisema wanafunzi wanaohitimu ni 148 kati yao wavulana ni 74 na wasichana 74 na wanafunzi 12 wamekosa kuhitimu kutokana na sababu mbalimbali.

Moses aliyataja mafanyikio wameweza kuchimba visima viwili vya kuhifadhia maji kwenye mabweni,kukalabati majengo,kutoa wanafunzi wa kidato cha nne na sita wanaojiunga na vyuo mbalimbali pia alitoa changamoto zinazoikumba shule ikiwemo  uhaba wa miundo mbinu ya majengo,upungufu wa watumishi,uhaba wa nyumba za walimu kwani hivi sasa kuna nyumba za walimu 11 na idadi ya walimu na watumishi ni 33,ukosefu wa usafi na ukosefu wa uzio eneo la shule hiyo.

Mmbaya ambaye katika hutuba yake kama mgeni rasmi aliwapongeza  wanafunzi wanaohitimu pia aliwaomba wanafunzi hao wajitahidi kusoma ili waweze kufanya vizuri kwenye mitihani na kuweza kutimiza malengo yaliyokuwa wenye tija kwao na kwa jamii.

Pia aliwasii na kuwaomba wananchi juu ya siku ya kupiga kura kuwachagua wagombea wanaowaona wanafaa bila kulazimishwa na mtu yeyote ili kuepuka mgawanyiko  kwani kuna maisha baada ya uchaguzi.


Post a Comment

 
Top