0


Mwaandishi wetu ,Nachingwea,
Wanachama wa mfuko wa afya ya jamii(CHF),wilayani Nachingwea,mkoani Lindi wamehakikishiwa upatikanaji mzuri wa huduma za afya kwa kuanzishiwa chumba maalumu kwenye hospitali ya wilaya  ambacho kitakuwa na waganga ambao watakuwa wanatoa huduma kwa wanachama hao pekee.
Hayo yalibainishwa na Kaimu mganga mkuu wa  halmashauri ya wilaya ya Nachingwea,Dr.John Sijaona wakati wa uzinduzi wa uhamasishaji  wa mfuko huo kwenye vijiji vinavyozunguka hospitali ya kanisa katoliki ya Mnero ambayo imeingia mkataba na halmashauri ya Nachingwea kuwahudumia wanachama wa CHF.
Dr.Sijaona alibinisha kuwa wanachama hao licha ya kuwa na waganga ambao watakuwa wanawahudumia pia ndani ya chumba hicho kutakuwa eneo la ambalo watapata dawa hapo hapo na kuwa kuna dawa za kutosha kwa ajili yao.
“Tumejipanga kikamilifu kuwahudumia hawa wanachama kwani licha ya kuwa na waganga pia chumba hicho kitakuwa na dirisha la dawa kwa wanachama”alisema Dr.Sijaona.
Aidha alibainisha kuwa kwenye vituo vya afya na zahanati  zote zenye wanachama  kuna dawa ambazo zimetendwa kwa ajili ya wanachama hao ambazo kila zinapokaribia kumalizika wahudumu wanatakiwa kupeleka maombi kwa mganga mkuu ambaye atawapatia kutoka kwenye bohari maalumu ambayo imeendaliwa kutunza dawa za wanachama wa CHF.
Akizungumza kwenye uzinduzi huo Katibu tawala wa wilaya ya Nachingwea.Saidi Moka amewataka watoa huduma kuwa lugha mzuri kwa wagonjwa ambao ni wanachama wa mfuko wa afya ya jamii na wale wa  Bima ya afya ili kuwafanya wasijutie kujiunga na mifuko hiyo.
Alisema wapo baadhi wa watoa huduma ambao hawazingatii maadili ya kazi yao kwa kuwatolea lugha chafu wanachama wa mifuko ya bima ya afya hali inayosababisha wananchi wengi wasijitokeze kwa wingi kujiunga na mifuko hiyo.   
Aliwahasa wakazi wanaozunguka Hosptali hiyo ya Mnero kujiunga kwa wingi kwenye  mfuko huo ili waweze kutumia fursa  hiyo ambayo ipo karibu  ambapo awali wanachama hao walilazimika kupata huduma ya matibabu kwenye vituo vya kutolea tiba vinavyomilikiwa na Halmashauri.
Naye Mwenyekiti wa kamati ya usimamizi wa hospitali hiyo ya Mnero Baba Ernest  Chikawe alisema kuwa wamejipanga kutoa huduma mzuri za afya kwa wanachama hao na kuitaka halmashauri kuwaongezea watumishi kwani kwa sasa kunaupungufu mkubwa wa watumishi hasa madaktari na wauguzi.
Hlmashauri ya wilaya  ya Nachingwea imeingia mkataba na hospitali ya Mnero wa kuwahudumia wanawake wajawazito,watoto chini ya miaka mitano na wanachama wa CHF wanaozunguka hospitali hiyo inayomikiwa na kanisa katoliki jimbo lla Lindi   ambapo halmashauri ndio inayolipia gharama hizo.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top