0


Afisa Habari wizara ya Nishati na Madini Badra Masudi akizungumza na waandishi wa habari  mkoa wa Lindi na Mtwara kwenye  mafunzo ya siku mbili yaliyoanza leo yanayohusu  Gesi na Mafuta
Na Athuman Cnani  na Frank Saidi Kilwa
Waandishi wa habari wa mikoa ya Lindi na Mtwara wameaswa  kuandika kwa kina habari za uchumi wa  gesi na mafuta ili ziweze kutoa elimu kwa wakazi wake itakayosaidia kukuza miradi ya maendeleo iliyoanzishwa na serikali hapa nchini.
Wito huo umetolewa na Dimara Tegambwage wakati wa mafunzo ya gesi na mafuta kwa waandishi wa habari kutoka mikoa ya Lindi na mtwara yaliyoandaliwa na wizara ya nishati na madini kwa lengo la kuwajengea uwezo wakati wa uandishi wao.
Amesema kufuatia matukio ya vurugu yaliyotokea mikoa ya lindi na mtwara waandishi wa mikoa hiyo wamekuwa wakishindwa kuripoti mara kwa mara habari za maendeleo hasa zile za uchumi wa gesi na mafuta ambayo kwa sasa imekuwa ni rasilimali kubwa kwa nchi yetu.
Aidha afisa habari wa wizara ya nishati na madini BADRA MASOUD amewataka wanahabari kuacha maswali ya kupikwa badala watumie taaluma yao kuhoji na kuandika habari walizofanyia uchunguzi wa kina.
Awali mwenyekitii wa chama cha waandishi wa habari  mkoani  Lindi  Abdulaziz Ahmadi alisema kuwa  mafunzo hayo ni muhimu  na yatasaidia waandishi kuwajengea uwezo wa kuandika habari za gesi na madini.
Abdul azizi aliitaka wizara ya nishati  na madini  kuangalia uwezekano  wa kutoa mafunzo hayo kwa uendelevu ili kuwafanya waandishi wa habari mikoa ya Lindi na Mtwara kuandika habari kwa uzalendo ,ukweli na usahii zaidi
Mafunzo hayo yanayofanyika wilayani kilwa mkoani Lindiyameandaliwa na wizara ili waandishi hao waweze kupata uelewa juu ya matumizi na faida za rasilimali gasi na mafuta baada ya kugundulika mkoani Mtwara.
 Mwnyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Lindi Abdulaziz Ahmadi akizungumza kwenye mafunzo ya uandishi wa habari za gesi na Madini iliyofadhiriwa na wizara ya nishati na Madini
 wanahabari wa mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwa mafunzoni
waandishi wa habari Lindi na Mtwara wakiwa kwenye mafunzo ya Gesi na mafuta yanayoendeshwa na wizara  ya nishati na madini yanayofanyika mkoani Lindi

Post a Comment

 
Top