0





Wafanyabiashara wa soko kuu Lindi mjini wamegoma kufungua soko wakishinikiza kumkataa Mtendaji  wa kata kwa kitendo cha kuwa mbabe ,kuwabambikia  madeni  ya  ushuru  na  kutotoa  risiti  za  malipo ya ushuru
Akizungumzia 
tukio  hilo  Mwenyekiti  wa  soko  Mohamedi  Matika  alisema  wameamua  kufunga  soko  kwa  lengo la  kushinikiza  uongozi  wa   Manispaa kumwondoa   mtendaji  wa   kata  kwa  kuto   toa  ushirikiano  kwa wafanyabiashara ubabe   na  kutotoa  risiti  za  ushuru  na  faini  zinazotozwa  kwa  wafanyabiashara.

Matika  Aliongeza  kuwa pamoja   kuwa wanalipa  ushuru  lakini  huduma  za  kijami ikiwemo   vyoo, usafi  haufanyiki katika   eneo  la  soko jambo  ambalo   wanadai  kuwa  faida  ya  kulipa  ushuru haina  maana kwenye  soko  hilo.
Kwa  upande wa  mtendaji  wa  kata  ya Matopeni  Omary  Salumu Nyemba   amekataa  tuhuma  hizo  na kueleza  kuwa wafanyabiashara  hawataki  kufuata utaratibu  na   kanuni  zilizowekwa  na  manispaaa  za kufanya  usafi  na kulipa  ushuru  kwa  hiari

Nyemba   aliongeza  kuwa kitendo  cha  kusimamia  sheria  na  kanuni  mara  kwa  mara kimetengeza  mazingira ya watu  kumchukia  na   kutoa  kauli  zisizo  faa  kwake   kwa  lengo  lakumtaka  kumzofisha  kiutendaji

Nae   kaimu  mkurugenzi  wa  manispaa  ya  Lindi Injinia    Endraw  Mayombo  alikiri  kutokea  kwa    tukio   la kufungwa  kwa  soko  hilo  na  kueleza  kuwa  wamewaomba  viongozi  kufungua  soko ili  wananchi  waendelee kupata  huduma    na  kuwataka  viongozi  wa  soko  kukaa pamoja  na  ofisi  yake kujadili  suala  hilo  sambamba  na kuwataka  watendaji  waliokusanya  ushuru kurejesha   fedha  kwa  wafanyabishara  hao.

Post a Comment

 
Top