0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakusudia kuimarisha Sekta ya Uvuvi katika azma yake ya kujenga uchumi imara  utakaostawisha maisha ya Wananchi wake.
                     
       
        Akizungumza na Ujumbe wa Viongozi wa Kampuni ya Uvuvi ya Hong Dong kutoka Nchini China ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Lan Ping Yong, Ofisini kwake katika  jengo la Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Amesema uimarishaji huo utaelekezwa zaidi katika ujenzi wa Viwanda Vidogo vidogo vya usindikaji wa mazao ya Baharini utakaotoa fursa ya kukaribisha Makampuni na Taasisi za Kimataifa kuwekeza miradi yao Visiwani Zanzibar.

Balozi Seif alimuahidi Mkurugenzi Mkuu huyo kuwa pande zinazohusika nchini zitakutana na kuangalia wazo la Kampuni hiyo la uwekezaji kwa lengo la kuchukuliwa hatua za muelekeo wa uanzishwaji wa uwekezaji huo.

Mapema Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Uvuvi ya Hong Dong ya Nchini China Bwana Lan Ping Yong amesema mradi wa Uvuvi unaotaka kuwekezwa Visiwani Zanzibar utakuwa na uwezo wa kutoa fursa za ajira zisizopungua elfu 1,700.

Ameongeza kuwa Taasisi hiyo imetenga nafasi Tatu kwa ajili ya Watendaji wa Sekta ya Uvuvi Zanzibar kwenda Nchini Mauritania kujifunza hatua iliyofikia ya Uwekezaji wa Kampuni  hiyo katika Nyanja ya Uvuvi.


        Wakati huo huo Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi mdogo wa India aliyepo Zanzibar Mhe. Barupal.

Post a Comment

 
Top