Waziri wa katiba na
sheria Tanzania Dkt.
Harrison Mwakyembe amesema sheria ya kumlinda mtoto ya Zanzibar pamoja na
ushahidi ni nzuri na itasaidia kupambana na na vitendo vya kijinsia.
Ametoa
pongezi hizo alipokutana na kuzungumza na waziri wa katiba, sheria, utawala
bora na utumishi wa umma Zanzibar Haroun
Ali Suleiman huko ofisini kwake mazizini mjini unguja.
Mhe. Mwakyembe
amesema sheria hiyo ipo tofauti na ile ya Tanzania bara,ambapo ameahidi kutumia nafasi hiyo kuangalia baadhi ya mambo kwa lengo la kuirekebishaSheria kumlinda mtoto ya Tanzania Bara.
Ameongeza kuwa sheria
ya ushahidi itasaidia kwa kiasi kikubwa kuona ushahidi unaotolewa na mtoto
unakubalika kwa ajili ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.
Nae waziri wa katiba, sheria, utawala bora na utumishi wa umma Zanzibar Haroun Ali Suleiman amesema baraza la wawakilishi limepitisha sheria ya ushahidi ambayo imeboreshwa zaidi kwa ajili ya kuutambua ushahidi
unaotolewa mahakamani na mtoto mdogo.
Aidha ameeleza kuwa baadhi
ya wahalifu na mahakimu wamekuwa wakipunguza ushahidi kwa kutumia mwanya hasa
pale unapotolewa na wwtoto chini ya miaka 18 pamoja na wenye ulemavu wa akili.

Post a Comment