Waziri wa biashara,
viwanda na masoko Zanzibar Balozi Amina Salum Ali amesema Zanzibar itaendelea
na mfumo wa ukaguzi wa magari kwa kushirikiana na nchi za kigeni hadi pale
yatakapofanyika mabadiliko ili Zanzibar kunufaika zaidi na mapato yanayotokana
na ukaguzi huo.
Kwa sasa shirika la
viwango Zanzibar ZBC hupata dola 25 kutokana na ukaguzi huo huku dola 125
zikienda katika nchi za kigeni.
Akitolea ufafanuzi swali la Mwakilishi wa
Jang’ombe Abdallah Diwani aliyetaka kufahamu kwanini ZBC inapata pesa kidogo za
ukaguzi ikilinganishwa na nchi za kigeni.
Mhe. Balozi Amina
amesema licha ya pato hilo kuwa dogo bado Serikali itaendelea kutumia utaratibu
huo mpaka pale yatakapofanyika marekebisho.
Pamoja
na hayo waziri huyo amezungumzia vifaa ambavyo tayari vimetumika vinavyoingizwa
nchini kuwa hufanyiwa ukaguzi wa kutosha kabla ya kuingizwa nchini.
Post a Comment