Umoja wa watu wenye
ulemavu Visiwani Zanzibar [UWZ] umeingia ubia na mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF katika
mradi wa ujenzi wa nyumba 16 za kupangisha zenye ghorofa nne kwa kila moja.
Akizungumza na
waandishi wa habari mwenyekiti wa umoja wa watu wenye ulemavu zanzibar Ali
omari makame ofisini kwake kikwajuni mjini Unguja, amesema mradi huo
utawasaidia kuwaingizia kipato.
Ameongeza kuwa mradi
huo ambao tayari umeridhiwa na Serikali utagharimu shilingi bilioni 30 mpaka kukamilika kwake.
Amefafanua kuwa mradi huo utakapokamilika UWZ
utakuwa ukipata asilimia 10 ya mapato huku ikikadidiriwa kupata milioni 36 kwa
mwaka.
Aidha amesema mradi huo
pia utajumuisha ukarabati wa mkubwa wa jengola ofisi ya uwz ili kuwa pahala
pazuri na muafaka na pa kufanyia kazi na penye mandhari nzuri..

Post a Comment