0


Mkuu wa mkoa wa mjini magharib Visiwani Zanzibar Mh  Ayoub Muhammed amewataka wananchi kuwasilisha maoni yao katika taasisi husika juu ya swala zima la kuanzishwa kwa mpango miji na vijiji Zanzibar.


        Akitia saini ramani ya mpango miji na vijiji pamoja na kuwakabidhi ramani hiyo wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa mabaraza ya manispaa, amesema mpango huo utaongeza thamani ya ardhi katika mkoa huo na kuwaweka watu wengi katika eneo moja.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Miji na Vijiji Zanzibar Muhammed  Juma amesema wananchi wamekuwa wakifanya ujenzi holela hali aliyoitaja kusababisha kizazi kijacho kukosa eneo la kujenga.
        Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Rahaleo mjini Unguja.
Kwa mujibu wa takwimu, mkoa wa mjini magharibi una wakazi laki 5 huku ikikadiriwa kuwa miaka 20 ijayo mkoa huo utakuwa na wakazi milioni moja na nusu.

Post a Comment

 
Top