BARAZA la manispaa
Zanzibar limeahidi kuendelea na zoezi la kukamata ng’ombe na mifugo mengine katika maeneo ya manispaa ya mji wa Zanzibar
linaendelea.
Hatua hiyo imekuja
baada ya siku za hivi karibuni kuripotiwa baadhi ya watu kuanza kurudisha
mifugo katika maeneo mbali mbali ya Manispaa hiyo licha ya kuwepo na marufuku ya kuzuwia mifugo
katika Manispaa hiyo.
Mkurugenzi wa baraza la
manispaa Zanzibar Mh Aboud Hassan Serenge amemwambia mwandishi wa blog hii kuwa tangu kuanza
kutekelezwa kwa marufuku hiyo, muonekano wa haiba ya manispaa ya mji wa
Zanzibar imeimarika.
Katika hatua nyengine Serenge amesema kuna baadhi ya maeneo ya Manispaa hiyo yalioonekana kupoteza ubora wake kwa sasa mambo yameimarika, huku akitolea mfano bustani na vipando vya wananchi
vinaonekana kustawi.

Post a Comment