WAKULIMA wa zao la korosho
nchini,wametekeleza agizo la Serikali kwa kuotesha na kupanda jumla ya miche
mipya 10,396,317,kwa kipindi cha miaka mitatu sasa,ikiwa ni moja ya kuwawezesha
kuondokana na umasikini wa kipato.
Kaimu mkurugenzi mkuu,Hassani Jarufu ameyaeleza
hayo,alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji,siku ya uzinduzi wa kampeni
ya kupanda mikorosho mipya msimu wa 2016/2017 iliyofanyika kijiji cha Chimbila
‘B’ Tarafa ya Mnacho,wilaya ya Ruangwa,mkoani Lindi,februari 10 mwaka huu.
Taarifa hiyo ilisomwa kwa niaba yake na kaimu
mkurugenzi wa Bodi ya korosho,Dustani Kaijage,ilieleza katika kipindi hicho cha
kuanzia 2013/14 hadi 2015/16,Serikali kupitia waziri mkuu Kassimu
Majaliwa,iliagiza kuoteshwa na kupandwa miche mipya mikorosho 10,000,000 kwa lengo
la kuongeza mapato ya mkulima na Taifa.
Kaijage alisema katika kipindi hicho,wakulima kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali,zikiwemo Halmashauri za wilaya na mikoa
inayolima zao hilo hapa nchini,wameweza kupanda na kuotesha miche mipya ya
mikorosho 10,396,317 sawa na asilimia 104% na hivyo kuvuka lengo lililokuwa
limewekwa.
Akaeleza kwamba katika kipindi hicho,miche 7,641,600
sawa na asilimia 74% ni mikorosho iliyopandwa kwa kutumia mbegu,wakati
2,754,717 sawa na asilimia 26% imepandwa kwa kutumia miche,na kwamba wahusika
wanaendelea kutunzwa.
“Umuhimu wa kupanda miche hii mipya unalenga
kuinua uzalishaji bora wa zao la korosho nchini,pamoja kutekleza agizo la
waziri mkuu wa Tanzania,Kassimu Majaliwa mwanzoni mwa mwaka jana”Alisema
Kaijage.
Kaimu mkurugenzi huyo alisema kutokana na agizo hilo
la Serikali, uongozi wa Bodi ya korosho nchini (CBT) iliingia mkataba na
vikundi (47) vilivyojishughulisha na uoteshaji mbegu ndani ya mkoa wa
Lindi,hivyo kuweza kupata miche 543,327 na kugaiwa kwa wakulima.
“Ni matarajio yetu kuwa ndani miaka (5) hadi (10) ya
uteklezaji wa mradi huu,uzalishaji wa korosho utaongezeka na kufikia tani
600,000,hivyo kuongeza mapato yatokanayo na zao hilo”Alisema Kaijage.
Mkuu wa mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi ambaye alikuwa
ndiyo mgeni rasmi katika uzinduzi huo,amewataka wakulima kutokubali kuwa
watumwa wa kilimo cha kubahatisha,badala yake waongeze nguvu katika kuzalisha
mazao mbalimbali,likiwemo zao la korosho,ili waweze kuondokana na umasikini
unaowakabiri.
Pia,Zambi ameiomba Bodi ya korosho kuharakisha
upelekaji mapema wa pembejeo,kwa wakulima ili waweze kuzitumia katika
kuzalishia mazao,kabla ya msimu haujawapita,sanjari na kuongeza vituo
vitakavyohusika na ugawaji wake,ili kuwaondolea usumbufu wa kufuatilia
huduma hiyo mbali na maeneo yao.
”Ninachokiomba kwenu Bodi ongezeni vituo,ili
kuwapunguzia wakulima mwendo mrefu wa kwenda Tandahimba kuzifuata hizi
pembejeo” Alisema Zambi.
Nae,mwenyekiti wa Bodi hiyo ya korosho Tanzania,Anna
Abdallah amelipokea ombi la kiongozi huyo wa mkoa wa Lindi,huku akihaidi
kukutana na watendaji wake,ili kulifanyika kazi,huku akiwahasa wakulima kuacha
kilimo cha kupanda miti isiyo na faida,badala yake wapande miti ya mikorosho
ambayo ina faida
Post a Comment