0
WANANCHI mjini Njombe wameilalamikia halmashauri ya Mji huo kuto pita kwa wakati kuondoa taka walizo kusanya tayari katika viroba kama ilivyo kawaida ya halmashauri hiyo kupitisha gari na kusababisha taka kutupwa maeneo mbalimbali ya barabara za mji.

Wamesema kuwa halmashauri awakli ilikuwa ikipitisha gari kwa wakati lakini kwa sasa gari haipiti kwa wakati na kusababisha baadhi ya wakati hao kukaa na taka kwa muda mrefu majumbani kwao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi hawa wanaomba halmashauri kuboresha mifumo ya uzoaji wa taka ama kurejesha vizimba kwa kuwa wapo tayari kulipia huduma ya kupitiwa na gari ya taka.

Halmashauri inasema kuwa iliweka mdhabuni kwaajili ya kuondoa taka mtaani lakini kuna matatizo kidogo na mdhabini huyo na amesimamishwa kwa muda wakati wapo kwenye mazungumzo.

Kwa upande wake mdhabuni anasema kuwa amesimamishwa kwa muda na halmashauri wakati wapo kwenye mazingumzo lakini pia fedha kutoka halmashauri zimekuwa zikichelewa ndio maana wamekuwa wakisuasua.

Halmashauri ya mji Njombe ilifanya utaratibu wa kuondoa taka mtaani kwa kufuta vizimba na huduma hiyo ilianza mwezi Julai na kuanza kusuasua mwezi novemba mwishoni kutokana na matatizo hayo lakini wakati huduma inaanza iliboresha usafi wa mazingira mjini.

Post a Comment

 
Top