0

Upinzani waomba mpatanishi mpya BurundiUpinzani nchini Burundi wafahamisha kuomba mpatanishi mpya kunako mzozo wa Burundi ambao kwa sasa unaelekea mwaka wa pili.
Vyama vya upinzani katika umoja wa CNARED  wamefahamisha kuwa mpatanishi Benjamin Mkapa ameonesha upande anaoegamia jambo ambalo ni kinyume na wadhifa aliopewa wa upatanishi.
Upinzani huo umemuomba rais wa Uganda Yoweri Museveni  kumteua mpatanishi mpya ili kupatia suluhu mzozo wa Burundi.
Kwa upande mwingine CNARED imeomba ushirikiano wa Umoja wa Afrika  na Umoja wa Mataifa  kutoa msaada wao kwa mpatanishi mpya.
CNARED iligoma kumtambua Benjamin Mkapa  baada ya kufanya ziara nchini Burundi Disemba 30 na kusema kuwa muhula wa 3 wa rais Nkurunziza ni haki yake kikatiba.
Watu zaidi ya 700 wamefariki tangu rais Nkurunziza kuteuliwa kuwania kiti cha urais Aprili 2015.
Vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi  vikidai kuwa ni kinyume na mkataba wa Arusha uliokomesha vita vya tangu mwaka 1993 hadi mwaka 2006.

Post a Comment

 
Top