0



Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano aliyemaliza muda wake, Job Ndugai.
 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano aliyemaliza muda wake, Job Ndugai, amesema timu zilizoundwa na Bunge kushughulikia vurugu za gesi zilizotokea mkoani Mtwara na mauji ya Kiteto, zilishamaliza kazi na kuwasilisha ripoti za uchunguzi kwa mamlaka husika.
 
Akizungumza na Nipashe , Ndugai alisema timu iliyoundwa na Bunge kuchunguza mauaji yaliyotokea Wilaya ya Kiteto  mkoani Manyara, iliongozwa na Askofu wa Kanisa la Mennonite, Amos Muhagachi.
 
Alisema timu hiyo ilifanya kazi kwa mwezi mmoja na walifanya utafiti uliohusu chimbuko la mauaji hayo pamoja na matatizo.
 
Ndugai alisema kuwa kuhusu timu iliyoundwa kuchunguza vurugu za geni zilizotokea mkoani Mtwara, timu hiyo nayo ilishakamilisha kazi yake na kuiwasilisha kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda, lakini haikusomwa bungeni na ilipelekwa moja kwa moja serikalini.
 
“Kimsingi timu zote hizo mbili zilizoundwa zilikamilisha kazi yake na kuwasilisha taarifa zao bungeni na Bunge lilipeleka moja kwa moja katika mamlaka husika,” alisema Ndugai.
 
Mwaka jana kulizuka mapigano baina ya wakulima na wafugaji yaliyosababisha vifo kadhaa. katika Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara.
 
Kutokana na hali hiyo, serikali iliunda timu ya watu 10 kutoka kada tofauti wakiwamo viongozi wa dini ambao walipewa jukumu la kufanya kazi ya usuluhishi kwenye vijiji vyenye migogoro wakiongozwa na Askofu Muhagachi.
 
Kadhalika, Mei 22, mwaka juzi, vurugu zilizotokea mkoani Mtwara, Bunge la Jamhuri ya Tanzania liliamua kuunda timu ya wabunge 13 Ikiongozwa na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Charles Mwijage.
 
Kamati hiyo ilipewa jukumu la kuchunguza chanzo cha vurugu hizo, kufuatilia hatua zilizochukuliwa na serikali kushughulikia mgogoro huo, kukutana na wadau wa sakata hilo na kuchunguza mambo mengine yenye uhusiano na mgogoro huo.
CHANZO: NIPASHE

Post a Comment

 
Top