Jumuiya
ya umoja wa wanawake Tanzania UWT,ya Chama cha Mapinduzi CCM -katika
Manispaa ya Mtwara Mikindani imelazimika kumjengea nyumba Bibi Rukia
Salehe mwenye umri wa miaka zaidi ya 75 ambaye amekuwa akilala nje kwa
miaka minne mfululizo licha ya juhudi zake za kuomba msaada kwa mamlaka
husika kushindikana.
Akizungumza
kwa masikitiko bibi Rukia Salehe anasema nyumba aliyokuwa akiishi hapo
awali ilianguka baada ya kuwa na nyufa nyingi,hivyo kukosa uwezo wa
kujenga nyumba nyingine,huku akisisitiza katika maisha yake hajawai
kupata mtoto licha ya kutumia muda mwingi kulea watoto wa ndugu na
marafiki lakini wameshindwa kumsaidia.
Akimzungumzia
bibi huyo mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Matopeni Omar Hussein
anasema licha ya bibi huyo kuomba msaada ofisi ya mkuu wa wilaya lakini
amegonga mwamba,hali iliyolazimu diwani wa Chama cha Mapinduzi kwa
kushirikiana na wanachama wa UWT kumsaidia ili kumuondoa katika
mazingira hatarishi.
Kibanda
cha bibi Rukia anachoishi ni hatarishi lakini amekuwa akikitumia kulala
kuhifadhi vitu vyake na kupikia huku mvua jua likimuwakia kutwa kucha.