0
Wawakilishi wanawake wamesisitizwa kujenga utamaduni wa kujiongezea maarifa na ufahamu katika masuala ya utawala ili kupanua demokrasia ndani ya Baraza la wawakilishi Zanzibar.

                                      baraza la wawakilishi zanzibar

          Akizungumza katika siku ya mwisho ya mafunzo ya siku nne ya kuwajengea uwezo wawakilishi wanawake, Naibu spika wa Baraza la wawakilishi Mgeni Hassan Juma amesema hatua hiyo itawasaidia wajumbe hao kijamii, kiuchumi na kisiasa.
          Amesema lengo  kuu  la  mafunzo  hayo  ni  kuwajengea  uwezo  wawakilishi  hao katika  maswala  ya  mawasiliano, kujitambua  hasa  pale  wanapojenga  hoja  katika  kuwasilisha   barazani  lakin  pia kuweza  kujiamin wakati wa  vikao  vya  ndani  na  nje.
          Nao washiriki wa mafunzo hayo wameeleza kunufaika kwa kupata muamko katika masuala ya kuchangia ndani ya vikao kutokana na kujifunza sheria na kanuni zinazolihusu Baraza la wawakilishi.

Mradi  huo  wa  mafunzo ya siku  4 unaoitwa  ujengaji  wa  uwezo  ulioshirikisha  wawakilishi  wanawake  Zanzibar  umedhaminiwa  na shirika la umoja wa mataifa la wanawake UN WOMEN. 

Post a Comment

 
Top