0
Imeelezwa kuwa licha ya uwepo wa asasi za kiraia zinazotoa elimu kwa jamii kuhusu masuala yanayohusu watu wenye ulemavu, bado baadhi ya watu wamekuwa wakiendelea kufanya vitendo vya udhalilishaji kwa jamii hiyo.

Mkuu wa mkoa wa mjini magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa 8 kwa watu wenye ulemavu wa akili kwenye ukumbi wa Skuli ya maandalizi Saateni mjini Unguja ambapo amezipongeza asasi hizo kwa elimu wanayoitoa kuhakikisha masuala ya udhalilishaji hasa kwa watu wenye ulemavu yanaondoka.
Nae mwakilishi wa watu wenye ulemavu Zanzibar Bi. Mwantatu amezitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili jamii ya watu wenye ulemavu wa akili nchini ni pamoja na wazazi wengine kutokutowa huduma bora za msingi kwa watoto wenye matatizo ya akili.
Mkutano huo wa siku moja umewashirikisha walimu kutoka katika skuli za Unguja na Pemba, watu wenye ulemavu na wadau wengine.



Post a Comment

 
Top