0
Kiasi cha sh. 25 milioni kimetengwa kwa ajili ya kukopesha  vikundi vya ushirika vilivyomo ndani ya jimbo la Chumbuni, visiwani Zanzibar

        Mwakilishi wa jimbo hilo Mhe. Miraj Kwanza amesema lengo la kutengwa kwa fedha hizo ni kuwasaidia wanajamii kuinua maisha yao kupitia vikundi vya ushirika.
        Mhe. Kwanza amesema tayari vikundi 56 vimepokea mafunzo ya wiki moja kutoka kwa wataalam wa masuala ya vikundi vya ushirika Zanzibar.

Aidha amewasihi wananchi wa jimbo la Chumbuni kuongeza ushirikiano ili kudumisha maendeleo ya jimbo lao kupitia vikundi vyao vya ushirika.

Post a Comment

 
Top