Na.Ahmad Mmow, Kilwa.
Kiwango kidogo cha ufaulu katika shule za msingi na sekondari Wilayani Kilwa mkoani Lindi kimetajwa kusababishwa na changamoto nyingi katika sekta ya elimu wilayani humo.
Kiwango kidogo cha ufaulu katika shule za msingi na sekondari Wilayani Kilwa mkoani Lindi kimetajwa kusababishwa na changamoto nyingi katika sekta ya elimu wilayani humo.
Hayo
yalielezwa jana mjini Kilwa masoko, na mtafiti wa shirika la Action
aid, Jacob Kateri wakati anawasilisha ripoti ya utafiti wa awali wa
mpango wa maendeleo ya elimu katika wilaya hiyo.
Kupitia mradi wa uwezeshaji elimu kwa kutumia rasilimali za ndani ya nchi.
Akisoma
ripoti hiyo kwa wadau wa elimu wa wilaya hiyo, Kateri alisema katika
utafiti huo uliowahusisha wadau waelimu ikiwawamo, walimu, wazazi na
wanafunzi.
Imebainika
kwamba sekta ya elimu wilayani humo inachangamoto nyingi zinazohitaji
kufanyiwa kazi na serikali kwa kushirikiana na jamii, ili kiwango cha
utoaji elimu kiboreke na kuongeza kiwango cha ufaulu.
Kateri
ambae shirika lake lilifanya utafiti huo kwa kushirikiana na mtandao wa
mashirika yasio ya kiserikali ya wilaya ya Kilwa(KINGONET) alizitaja
changamoto hizo kuwa ni wazazi kutojua umuhimu wa elimu, umasikini na
kilimo cha kuhamahama.
Alisema umasikini wakipato kwa wazazi wilayani humo unasababisha washindwe kuwapatia watoto wao mahitaji muhimu na yalazima.
Ambapo baadhi ya wazazi wanawatumia watoto katika shughuli na kazi za uzalishaji mali badala ya kuwahimiza waende shuleni.
Alisema
licha ya umasikini lakini pia jamii wilayani humo haitambui umuhimu wa
elimu hivyo kushindwa kushiriki na kuchangia kuinua kiwango cha elimu.
Ikiwamo kujitolea kujenga nyumba za walimu, vyoo na madarasa.
"Kilimo
cha kuhamahama pia kinasababisha wazazi kushindwa kuwasimamia kwa
karibu watoto wao, na wengine wanahama nao nakusababisha washindwe
kuhudhuria shuleni," alisema Kateri.
Kateri
alibainisha kuwa kiwango cha watoto kuacha shule ni 3.5% ya watoto wote
walioandikishwa. Kati yao wavulana wakiwa 4.2% na wasichana 2.3%.
Ambapo
katika utafiti huo imebainika katika shule 15 zilizohusishwa na utafiti
huo imebainika kuwa ingawa uwiano unatakiwa tundu moja kutumiwa na
wavulana 20 na 25 kwa wanawake, lakini wilayani humo uwiano ni tundu
moja kwa wavulana 61, na 55 kwa wasichana walio andikishwa. Kati yao wavulana wakiwa 4.2% na wasichana 2.3%.
Ambapo
imeelezwa wakati wavulana wakiacha shule kwasababu ya kufanya biashara
kwenye vituo vya mabasi na shuguli za uvuvi. Wasichana kwa upande wao
wanaacha shule kutokana na ushawishi wa wazazi kuwatumia kwa kazi ndani
na ajira za kazi ndani mijini.
Kateri
aliendelea kusema upungufu wa walimu katika wilaya hiyo ni mkubwa kiasi
cha kusababisha baadhi ya shule za msingi kuwa na wastani wa mwalimu
mmoja kwa wanafunzi 81.
Aidha
Kateri alibainisha tatizo la uhaba wa vyoo ambao unasababisha wanafunzi
kukosa utulivu kutokana na kutokuwa na uhakika wa kwenda kujisaidia
wawapo shuleni.
Kuhusu uandikishaji wawatoto katika madarasa yote, mtafiti huyo alisema kiwango cha uandikishaji kimeongezeka.
Akibainisha
kwamba ongezeko la uandikishaji toka mwaka 2015 na mwaka 2016 ni 7.8%
bila kujali jinsia. Ambapo uandikishaji kwa darasa la kwanza
umeongezeka kwa 50% kwa mwaka 2016, wavulana walioandikishwa wakiwa 61%
na wasichana 37%.
Hata hivyo alisema watoto wa umri wa kuwa shuleni ambao bado wapo nje ya shule ni 3.6% ya wanafunzi wote.
Huku 3.5% wakiwa wasichana na 3.6% ni wavulana.
"Shule zinazokadiriwa kuwa na watoto wengi wa umri wa kuwa shuleni ambao wapo nje ya shule ni Lihimalyao, Nandembo na Mingumbi.
Hata
hivyo adhabu ya viboko inaongoza kwani kati ya shule 15, shule 14
zimesema ni suala la kawaida, huku ikifuatiwa na ukatili wa kimwili
ambopo shule nne wamesema nikawaida" ukatili wa kingono nao umetajwa
katika shule tatu, moja ikisema umetokea mara chache na kumi zimesema
haujatokea," alisema Kateri.
Kwa
upande wake mkuu wilaya hiyo, Christopher Ngubiagai licha ya kuipongeza
halmashauri ya wilaya kupitia idara ya elimu ya shule ya msingi kwa
kupandisha kiwango cha ufaulu wilayani humo kutoka 33% mwaka 2013 hadi
kufikia 56% mwaka jana.
Alisema tatizo la upungufu wa walimu nikubwa ambapo wilaya hiyo inaupungufu wa walimu 307 wa shule za msingi.
Ngubiagai
aliwataka walimu kuishi katika vituo vyao vyakazi badala ya nje ya
vituo vyao. Huku akihaidi kuwazawadia baiskeli walimu ambao shule zao
zitakuwa na matokeo mazuri ya ufaulu.
Post a Comment