0
 
Ni vita kwa Simba iliyo katika nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 16 inaposaka ushindi na pointi tatu leo dhidi ya Coastal Union ya Tanga ili ipande kwa mara ya kwanza na kuingia tatu bora.
Simba haijagusa tano bora kwenye msimamo, ila kama itashinda leo itavunja mwiko kama ilivyotokea kwa Yanga ilipoifunga Coastal Union 1-0 Jumatano na kukaa kileleni kwa mara ya kwanza.
Timu hiyo inaikabili Coastal Union ugenini kwenye Uwanja wa Mkwakani, ikiwa na lengo la kushinda na kupanda juu.
Mechi nyingine za leo zitakuwa ni; JKT Ruvu na Mbeya City kwenye Uwanja wa Azam Complex, Ruvu Shooting, ugenini kuikabili Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, Ndanda wataikaribisha Stand United, Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara na Kagera Sugar wakiwa uwanja wao mpya, Kambarage Shinyanga kuikabili Mgambo JKT.
Hata hivyo, haitakuwa kazi rahisi kwa Simba kushinda leo dhidi ya Wagosi wa Kaya, ambao wanaugulia maumivu ya kufungwa 1-0 na Yanga na hawako tayari kupoteza mchezo mwingine kirahisi, wakiwa nyumbani.
Kocha Goran Kopunovic alisema mechi hiyo itakuwa ngumu kwani wapinzani wao wanatumia mabavu uwanjani, lakini watapambana ili kuhakikisha wanaibuka na ushindi.
Kopunovic aliisoma Coastal Union wakati ikicheza na Yanga, ambako aligundua mambo kadhaa, likiwamo la jinsi timu hiyo inavyocheza soka la nguvu na ubabe.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top