Mtu mmoja ambaye hakufahamika jina lake ametaka kujiua kwa kujitupa
chini baada ya kupanda kwenye Daraja la Ubongo kituo cha mabasi ya Mkoa.
Mtu huyo ambaye hakufahamika kama ni mgonjwa wa akili au kachoka kuishi
tu amekuwa ni kituko katika eneo hilo la Ubungo baada ya kutaka
kujirusha kwenye Daraja kwa lengo la kujiua.
Hata hivyo haikufahamika kilicho msibu mtu huyo mpaka akaamua kutaka
kujiua, Hata hivyo Polisi walifika Eneo la Tukio na kufanikiwa kumshusha
Chini na kumpeleka katika kituo cha polisi Urafiki..