0




Mwaandishi wetu LIWALE

WANANCHI wilayani Liwale mkoani Lindi wameshauriwa kuanza utamaduni wa kuvuna  maji ya mvua kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, uzalishaji wa mazao  ya kilimo na mifugo.

Wito huo umetolewa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Gaudes Nyamiula wakati alipokuwa anafungua  semina ya wataalam kuhusu uratibu wa utekelezaji miradi ya ajira ya muda chini ya mpango wa kunusuru kaya maskini Tasaf awamu ya tatu katika ukumbi wa kituo cha walimu wilayani humo.

Nyamiula  alisema sehemu kubwa ya wilaya  Liwale inapata mvua za wastani  na sehemu nyingine mvua za kutosha  lakini hata hivyo wananchi wameshidwa kutumia  maji ya mvua  kwa faida ikiwemo kwenye miradi ya uzalishaji , kilimo na mifugo.

Aidha mkurugenzi huyo amewataka washiriki kuwa wavumilivu na kuacha tabia ya kuvaa kofia kutoa  maamuzi  bali wakaziwezeshe  jamii kutambua  vipaumbele  vinavyogusa maisha  yao ya kila siku na vizazi vijavyo.

Kwa upande Afisa maendeleo ya jamii kutoka Tasaf makao makuu Amos Mkude alisema lengo kubwa la warsha hiyo  ni kutoa  mafunzo  ya timu ya  wawezeshaji  kwenye  maeneo ya utekelezaji kuhusu miradi ya kutoa ajira ya  muda ili waweze kuwaelimisha  jamii hatua zitakazo takiwa kufuatwa ili walengwa wapate ajira ya muda  na kuongeza mapato.





Wanafanyakazi wa vitengo mbalimbali wa Halmashauri wilaya wakiwa kwenye semina ya wataalam kuhusu uratibu wa utekelezaji miradi ya ajira ya  muda chini ya mpango wa kunusuru kaya maskini Tasaf awamu ya tatu katika ukumbi wa kituo cha walimu wilayani humo.

Post a Comment

 
Top