0
                                          Timu ya taifa ya Ghana.
Timu ya Taifa Ghana imekua timu ya tatu kufanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la mataifa ya Afrika baada ya kuibanjua Guinea kwa mabao 3-0.
Winga Christian Atsu ndie alienza kuipatia Ghana bao la kwanza dakika ya 4 ya mchezo kabla ya kuongeza tena bao la pili dakika ya 61.
Appiah akashindilia msumari wa mwisho kwa kufunga bao la tatu lilifugwa dakika za lala salama za mchezo.
Guinea walipata pigo katika dakika za mwisho kwa kipa wao Naby Yattara kupewa kadi nyekundi kwa kumchezea rafu mshambuliaji Asamoah Gyan.
Kwa ushindi huo Ghana au maarufu kwa jina la black Star watachuana na wenyeji Guinea ya Ikweta katika mchezo wa nusu fainali utakaopigwa katika dimba la Estadio De Malabo.

Post a Comment

 
Top