0
PICHA KUTOKA MAKITABA

Mwaandishi wetu Liwale….
Wananchi wa  kata ya Kipule  kijiji cha  Makinda wilaya  Liwale  mkoani Lindi wamemtimua mbunge wa viti maalum,zainabu  Kawawa  kwa  madai  kufanya mkutano wa kutangaza nia ya kuomba ubunge katika jimbo hilo kabla ya  muda wa kufanya hivyo haujafika.
Tukio hilo limetokea juzi(alhamisi)  majira ya saa nane  mchana baada ya mbunge huyo kufika kijijini hapo kwa lengo la kukutana na  mwenyekiti wa kijiji Salum Kachwele ili kumtaka  aitishe  mkutano wa wajumbe wa serikali ya kijiji na baadhi ya wananchi hasa wazee maarufu ikiwa ni kuwashaawishi ili wamwuunge mkono katika harakati zake za kuwania ubunge wa jimbo hilo.
Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Salum Kachwele alisema mbunge huyo alifika kijiji hapo akiwa na mpambe wake Mkopora Mkopara  na   kumuomba awaite  wajumbe wa serikali  ya kijiji  pamoja na wazee maarufu ili azungumze nao jambo ambalo alidai hakulikubali kwani kabla ya harakati hizo za ubunge Kawawa hajawahi kufanya kikao chochote wala kutembelea katika kijiji hicho.
Kachwela alisema  kabla zoezi la kukutana na wanachi hao  halijafanikiwa lilikuja kundi  kubwa la wananchi likiongozwa na vijana wakizomea wakiwa na mawe na magongo waliotokea kwenye mkutano wa chama cha wananchi cuf waliokuwa kwenye mkutano wakuwashukuru wananchi kwa kukichangua cha hicho kwenye uchagunzi wa serikali uliopita  na kumtaka mbunge huyo kuondoka katika eneo  mara moja.
 Kwa upande wake mbunge  Zainabu kawawa alikiri kutembelea kijiji hapo ila alikataa kufanya kikao na wananchi hao  na kutokea tukio la kufukuzwa na kueleza kuwa yeye alikwenda kufanya ziara ya kikazi ya kuwatembelea wapiga kura kuhamasisha maendeleo.
 ‘Ndugu  yangu hayo maneno sio kweli mimi nilikwenda kijiji hapo kufanya kazi za kibunge sio kufanya kampeni kama ilivyoelezwa na hao watu wasionitakia mema’ukweli ni kwamba  mti wenye matunda matamu ndiyo unapigwa mawe alisema Kawawa.SAUTI YA KUSINI

Post a Comment

 
Top