0

Mwaandishi wetu Liwale
MKAZI wa kijiji cha Kibutuka,wilaya ya Liwale,mkoani Lindi, Mustafa Kinyuwile (40) amekufa papo hapo,baada ya kushambuliwa na tembo,alipokuwa na wenzake wakiwinda wanyama katika msitu wa hifadhi ya maliasili wa Serou.
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoani hapa,Renatha Mzinga,akizungumza ba waandishi wa habari alisema kuwa Kinyuwile alikutwa na mkasa huo,Decemba 31/2014,saa 8:15 mchana ambapo waliingia kwenye hifadhi hiyo bila ya kuwa na kibari kinachowaruhusu kufanya hivyo kutoka mamlaka husika.
.
Mzinga alisema siku hiyo,Kinyuwile akiwa na wenzake wawili, aliowataja kuwa ni,Chande Mtabiaga na Mateso,walikuwa kwenye msitu huo wakifanya shughuli za uwindaji kwenye msitu huo wa Hifadhi,ndipo tembo huyo aliyekuwa katika himaya yake alianza kuwafukuza  na kufanikiwa kumpata mmoja wao.
Alibainisha kuwa baada ya Kinyuwile kuuawa na tembo huyo,  Mtabiaga na Mateso waliuchukuwa mwili wa mwenzao kisha kuutelekeza eneo la kijiji cha Kilangala,badala ya nyumbani kwake na wao kuondoka kusikojulikana.
“Huyu mwili wa huyu marehemu ulikutwa umetupwa eneo la kijiji cha Kilangala,huku umenyofolewa jicho la kulia na mbavu zake zikiwa zimepondwa pondwa”Alisema Kamanda Mzinga.
Kamanda Mzinga alisema katika ufuatiliaji wao wa awali jeshi la polisi limebaini wawindaji hao,walikuwa wakifadhiriwa na mfanyabiashara wa vifaa vya pikipiki aliyemtaja kuwa ni,Kasimu Mtabiaga (51) ambaye ni ndugu watu aliokuwa akishirikiana na marehemu Kinyuwile katika shughuli zao za uwindaji.
Amesema tayari wanamshikilia mfanyabiashara huyo kwa mahojiano zaidi,huku akisubiri taratibu zingine za kisheria.
“Kwa sasa jeshimletu linamshikilia  kaka yake marehemu  kwa mahojiano zaidi,ikiwa ni pamoja na kutuwezesha kuwapata hawa wenzake,ili sheria iweze kuchukuwa mkondo wake”Alisema Mzinga.
Kamanda huyo wa Polisi mkoani Lindi,Renatha Mzinga amezidi kutoa wito kwa kuwataka wananchi kuacha tabia ya kuwinda bila ya kufuata utaratibu uliowekwa na Serikali.KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPAHAPA

Post a Comment

 
Top