0

                           PICHA KWA HISANI YA FAHARI YA KUSINI


mwaandishi wetu Somanga

Ujenzi wa barabara ya  Kilometa  60 kati Ndundu Rufiji hadi Somanga wilayani Kilwa kwa kiwango cha Lami  kwa kutumia fedha za mapato ya ndani zilisababisha nchi ya Kuwait kurejea tena na kushirikiana na serikali kujenga barabara hiyo baada ya awali kutotoa Fedha licha ahadi
Hayo yameelezwa  na   Katibu Mkuu  wa Wizara ya Ujenzi,Mhandisi Mussa Iyombe wakati wa Ukaguzi  wa barabara hiyo uliofanyika kijijini Somanga wilaya ya Kilwa mkoani Lindi.
Mhandisi Lyombe alisema nchi ya Kuwait ilisita kuendelea kufadhili ujenzi barabara hiyo yenye urefu wa kimometa 60,serikali iliendelea na ujenzi kwa kutumia fedha za ndani Ambapo awali ilikadiriwa ujenzi huo  ungegharimu shilingi bilioni 58 Ha ta hivyo kutokana na ujenzi huo kuchelewa kukamilika, gharama ilipanda na kufikia shilingi bilioni 66 hadi kukamilika.
Pamoja na kuruhusu kutumika kwa barabara hiyo baada ya kuunganishwa kati ya kijiji cha Marendego na Somanga Iyombe aliwaasa watumiaji wa barabara hiyo  ikiwamo madereva na watembea kwa miguu kuitunza barabara hiyo ambapo  Kwa upande wao baadhi ya madereva licha ya kuishukuru serikali kwa kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo huku wengine wakiomba kutengenezwa kwa barabara zingine zinazounganisha Wilaya hata kwa kiwango cha changarawe ikiwamo barabara ya Ruangwa hadi Lindi,Nachingwea hadi Nanganga na Masasi hadi Nachingwea kuanganisha na Wilaya ya Liwale

Awali Meneja wa wakala wa Barabara(Tanroads) mkoa wa Lindi Mhandisi Issack Mwanawima alieleza furaha yake baada ya kukamilika kwa  barabara hiyo ya km 60 iliyojengwa Kwa zaidi ya Miaka 5 Toka ujenzi Uanze. SOMA HAPA BOFYA

Post a Comment

 
Top