Cristiano
Ronaldo ameandika historia nyingine katika kitabu cha rekodi cha Real
Madrid baada ya kufunga magoli mawili katika ushindi wa 3-0 waliovuna
dhidi ya Getafe jioni kwenye mechi ya La Liga.
Hakuna
mchezaji yoyote katika historia ya Real aliyefunga magoli mengi ya
ugenini kumzidi Ronaldo ambaye amefunga mabao 27 na 28 katika msimu wa
ligi.
Gareth
Bale pia aliifungia Real Madrid dakika za lala salama, ingawa wakali
hao wa Bernabeu walikwenda mapumziko bila kufunga goli.
Post a Comment