0



wajumbe wa baraza la madiwani halmashauri ya wilaya Ruangwa wakiwa kwenye kikao  cha bajeti

Mwandishi wetu Ruangwa


 BARAZA la madiwani Halmashauri ya Wilaya  Ruangwa Mkoani Lindi  limepitisha bajeti ya zaidi ya sh bilioni 20 zitakazokusanywa na kuelekezwa katika utekelezaji wa miradi  ya maendeleo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2015/2016.

Kati ya kiasi hicho cha fedha,sh bilioni 1.627 zinatarajiwa kukusanywa kutoka kwenye vyanzo vyake mbalimbali vya mapato ya ndani ambapo ruzuku kutoka serikali kuu na misaada kutoka kwa wafadhili ikitarajiwa kuwa ni zaidi ya sh bilioni 4.8
Akisoma taarifa ya mapendekezo ya mpango wa maendeleo na bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa mwaka wa fedha mwaka 2015/2016 katika mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Ruben Mfune alisema makadilio ya bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2015/2016 ni sh bilioni 20.361
Alisema makadilio hayo yamepanda kutoka sh bilioni 15.279 kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015 ingawa hadi kufikia Novemba 2014,Halamashauri hiyo ilifanikiwa kukusanya jumla sh bilioni 5.657 kutokjana na vyanzo vya ndani sawa na asilimia 34 ya makadilio yake.
Kwa mujibu wa mfune Halmashauri inatarajia kutumia bilioni 4.885 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kutumia vyanzo mapato kama vile ruzuku kutoka serikali kuu,vyanzo vya ndani pamoja na fedha kutoka kwenye programu za Elimu  Sekondari (SEDP),Maji na Usafi (NWSSP) pamoja na Mfuko wa Barabara.
Alisema licha ya kupitisha makisio ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2015/2016 Halmashauri hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo huathiri utekelezaji  wa malengo wa utekelezaji yanayowekwa kama vile kucheleweshwa kwa fedha za ruzuku kutoka serikali kuu, pamoja kutofikiwa kwa malengo ya  ukusanyaji mapato kwenye baadhi ya vyanzo vya Halmashauri.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Ruangwa  mkoani Lindi Ruben Mfune akifafanua jambo kwenye kikao cha baraza la  madiwani cha bajeti kilichofanyika hivi karibu kushoto kwake ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo Isa Libaba na makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

Post a Comment

 
Top