Mwaandishi wetu Lindi
kamanda wa polisi mkoa wa Lindi Renata mzinga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari
SERIKALI
Mkoani Lindi imetaka Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kubomoa vibanda vyote vilivyojengwa nje ya
utaratuibu mara moja.
Agizo hilo
lilitolewa jana na mkuu wa Mkoa wa Lindi,Mwantumu Mahiza wakatinalipokuwa
akizungunza kwenye baraza maalumu la Madiwani wa Manispaa hiyo,alisema kuwa ni
muhimu vibanda hivyo kubomolewa mara moja na watendaji wa mamlaka hiyo.
Natoa agizo
hilo mara moja litekelezwe kwani
litasababisha kuleta vurumai kwa ujenzi holela,na hata kama sisiviongozi tuna
vibanda vyetu,alisema Mahiza.
Alisema
maofisa mipango miji,Mkurugenzi hakakikisheni kazi hiyo inafanyika kwa wakati
unaotakiwa si tena kuleta kesho keshokutwa.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
Asha Kigoleche alisema kuwa tatizo lipo katika baraza la Madiwani.
Alisema
baadhi ya viongozi hususani haswa Madiwani na Mbunge mmoja wana vibanda vyao
vilivyojengwa nje ya utaratibu ,lakini mpaka sasa havijabomolewa.
Alisema
watendaji nao walishapewa taarifa nao wanasita kwani kuna kiongozi naye ni
Mbunge naye alikiuka taratibu hizo za ujenzi.
Mwenyekiti
huyo alisema hivi karibuni vilibomolewa baadhi ya vibanda vya madiwani
vipatavyo saba.
Alisema kwa hiyo kutokana na ubomoaji huo sheria
ni msumeno lazima nao wabomolewe.
Post a Comment