0

mwenyekiti wa kikao cha barabara mkuu wa mkoa wa Lindi Mwamtumu Mahiza akifungua kikao hicho kwa kuwataka wajumbe kuwa wasikivu na kuchangaia kwa umakini.

mwaandishi wetu Lindi……

Wakala wa barabara mkoani Lindi wameombwa kuziangalia   barabara zao za zilizoko wilayani  Ruangwa  ili kunusuru maisha ya  watu na  mali zao.
Ombi hilo limetolewa  na mkuu wa wilaya Ruangwa Agnes Hokororo kwenye kikao cha bodi ya barabara  kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Lindi
Hokororo alisema  barabara ya Nanganga kwenda wilayani  Ruangwa ipo katika hali mbaya  na madaraja yana matatizo  na baadhi ya maeneo katika barabara hiyo yamegeuka kuwa njia ya maji na makazi ya watu yapo mashakani.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Isa Libaba alisema barabara zinazohudumiwa na Tanroad zinahitaji  matengenezo , hivyo ni vyema wataalamu na watendaji wa mamlaka hiyo wakatembelea barabara hizo kujionea hali halisi ya uharibifu  unaofanywa na mvua za masika zinazoendelea kunyesha.
Kwa upande wake meneja wa Tanroad mkoa wa Lindi injinia Isack Mwanawimba alisema kuwa  ofisi yake inatambua kuwepo kwa matatizo madogomdogo  wakati huu wa masika na ufanya marekebisho  ya haraka kwenye maeneo ya barabara yanayoaribiwa na mvua ili kuwafanya watu waendelee kutumia
 Mwenyekiti wa halmashauri ya Nachingwea MR Chikawe mjumbe wa kikao cha bodi ya barabara mkoani Lindi akizungumzia kuhusu matengenezo ya mara kwa mara ya barabra za TanRoad zilizoko wilayani Nachingwea.
 


Post a Comment

 
Top