Image captionMugabe alijiuzulu nafasi ya urais Novemba mwaka jana baada ya shinikizo la jeshi la nchi hiyo
Aliyekua Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amevunja ukimya kwa mara ya kwanza tangu aondolewe Madarakani, amesema kuwa amekua muhanga wa mapinduzi ya kijeshi.
Akiongea na televisheni ya SABC ya Afrika kusini Mugabe amesema kuwa Rais wa sasa Emerson Mnangagwa asingeweza kuingia madarakani bila kutumika kwa jeshi.
Akiwa katika nyumba yake ya kifahari mjini Harare Mugabe amekemea mbinu zilizotumika kumuondoa madarakani.
Amesema alikua tayari kufanya mazungumzo na Rais wa sasa Emerson mnangagwa na angehakikisha mabadiliko ya madaraka ya uhalali na si yale ya kulazimishwa.
Mugabe amesema kuwa Yuko tayari kwa ajili ya Mazugumzo na Mnangagwa ili kulinda katiba yao.
Image captionMnangagwa alikuwa makamu Rais wakati Mugabe akiitawala Zimbabwe
Hakuna uhakika kama rais huyo wa zamani mwenye Umri wa miaka 94 Anataka kurudi madarakani ama la, lakini ni wazi kuwa anadhani amesalitiwa na rais wa sasa Emerson Mnangagwa.
Amesema kuwa hakudhani kama angepoteza imani yake kwa Mnangagwa kwani yeye ndie alimsaidia kuingia serikalini.
''siamini kama yeye Mnangagwa angeweza kuniondoa madaraki , nimemuingiza serikalini, nimemsaidia alipokua jela anataka kunyongwa, sikuwaza kabisa kama siku moja yeye ndio atakua mtu wa kunitoa madarakani''
Aidha Mugabe ameogeza kuwa madaraka ya sasa yameingia kwa njia zisizo halali.
Image captionJeshi la Zimbabwe lilichangia pakubwa kumuondoa Mugabe madarakani
''Lazima tufute aibu hii, ambayo tumejiletea wenyewe, hatuistahili, hatuistahili, hatuistahili , tafadhali hatuistahili kabisa.Tunatakiwa kuwa nchi inayoheshimu katiba, ndio tunaweza kuwa na mapungufu hapa na pale lakini bado lazima tuheshimu sheria.''
Katika mitandao mbalimbali ya kijamii, baadhi ya wazimbabwe wanashangazwa na mkongwe huyo wa miaka 94, na wengine wanaamini kuwa amepoteza uhalisia kabisa baada ya kuongoza kwa miaka 38 , wakati wake sasa umekwisha.
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Ki...Read more »
kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa...Read more »
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHuenda ndege zikatengezwa bila madirisha katika siku za usoni.
Kampuni ya ndege ya Emirates imezindua nd...Read more »
Image captionMaandamano yamefanyika mjini Nairobi siku ya Jumatatu kulalamika kuhusu tuhuma za ubakaji katika shule ya Moi Girls Nairobi
Walimu pamoj...Read more »
Operesheni ya mwisho ya Tundu Lissu imefanyika na kumalizika salama.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alifanyiwa op...Read more »
Haki miliki ya pichaAFPImage captionBado muswada unahitaji kupitishwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame kabla ya kuanza kufanya kazi.
Bunge nchini Rwanda...Read more »
Post a Comment
aprieztmkrdezign
218168578325095
Emoticon
Click to see the code! To insert emoticon you must added at least one space before the code.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.