Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionMaandamano dhidi ya serikali nchini Ethiopia
Serikali ya Ethiopia imetangaza hali ya tahadhari siku moja baada ya waziri mkuu kujiuzulu.
Taarifa iliotolewa na runinga ya taifa imesema kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kukabiliana misururu ya maandamano dhidi ya serikali ambayo yamelikumba taifa hilo.
Makumi ya watu wameuawa na wengine zaidi kujeruhiwa wakati wa maandamano hayo yalioitishwa kupigania kuwachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa.
Ni mara ya pili serikali hiyo imeweka hali ya tahadhari kukabiliana na ghasia hizo.
Kulingana na mwandishi wa habari wa BBC Emmanuel Igunza tangazo hilo lilifanywa kwa mara ya kwanza katika ukurasa wa facebook wa chombo hicho cha taifa.
Lakini taarifa hiyo haikutoa muda utakaochukuliwa na tahadhari hiyo ama masharti ya kuwepo kwake.
Inajiri siku moja baada ya waziri mkuu Hailemariam Desalegn kutangaza kuwa anajiuzulu kutokana na mzozo ambao umekabili kipindi chake cha uongozi.
Bunge linatatarajiwa kutoka katika likizo ili kuidhinisha kujiuzulu kwake ambako tayari kumeungwa mkono na chama tawala.
Image captionAliyekuwa waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn
Taifa la Ethiopia limekabiliwa na zaidi ya miaka mitatu ya maandamano dhidi ya serikali katika maeneo tofauti ikiwemo eneo la Oromia ambalo ndio kubwa zaidi nchini humo.
Miongoni mwa mahitaji yake ni mabadiliko ya kisiasa , haki za umiliki wa ardhi na kuachiliwa kwa wanasiasa waliofungwa.
Wiki iliopita serikali iliiwaachilia huru mamia ya wanasiasa wa upinzani na waandishi lakini maandamano yameendelea.
Mnamo mwezi Oktoba 2016, serikali ilitangaza hali ya tahadhari iliochukua miezi 10.
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Ki...Read more »
kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa...Read more »
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHuenda ndege zikatengezwa bila madirisha katika siku za usoni.
Kampuni ya ndege ya Emirates imezindua nd...Read more »
Image captionMaandamano yamefanyika mjini Nairobi siku ya Jumatatu kulalamika kuhusu tuhuma za ubakaji katika shule ya Moi Girls Nairobi
Walimu pamoj...Read more »
Operesheni ya mwisho ya Tundu Lissu imefanyika na kumalizika salama.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alifanyiwa op...Read more »
Haki miliki ya pichaAFPImage captionBado muswada unahitaji kupitishwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame kabla ya kuanza kufanya kazi.
Bunge nchini Rwanda...Read more »
Post a Comment
aprieztmkrdezign
218168578325095
Emoticon
Click to see the code! To insert emoticon you must added at least one space before the code.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.