0
Rais wa Sudan kusin,Salva Kiir
Image captionRais wa Sudan kusin,Salva Kiir
Kumekuwa na maandamano katika miji mbalimbali nchini Sudan Kusini mara baada ya gharama ya mkate kuongezeka mara mbili zaidi.
Hatua hiyo ya maandamano imekuja baada ya serikali ya nchi hiyo kufanya maamuzi ya kuondoa ruzuku ya vyakula na kusababisha gharama ya mkate kuwa kubwa mara dufu.
Huko magharibi mwa Darfur, mwanafunzi mmoja aliyekuwa katika maandamano aliuwawa na wengine sita kujeruhiwa mara baada ya maandamano hayo kugeuka kuwa ya fujo.
kusin
Image captionRamani inavyoonesha Sudan kusini
Katika mji mkuu wa Khartoum, polisi walitumia mabomu ya machozi kusambaratisha watu ambao walikuwa wamefunga barabara na kuchoma matairi.
Naibu waziri wa mambo ya ndani alikanusha kuwa maandamano hayo hayakutoea kutokana na ongezeko la bei na kuahidi kuwa atawashughulikia wale wote waliokuwa wanafanya maandamano yenye fujo.
Serikali ya Sudan pia imezuia magazeti yote yaliyokosoa ongezeko la bei kutouzwa.
Maamuzi ya kuongeza bei ya mkate kwa serikali ya Sudan ni sehemu ya kufuata matakwa ya IMF ili kukuza uchumi wa nchi hiyo.

Post a Comment

 
Top