Wanajeshi wa Iran, wamewatisha wandamanaji wanaopinga serikali, kwamba jeshi litatumia nguvu nyingi, iwapo fujo za kisiasa zitaendelea.
Ilani hiyo imetolewa baada ya usiku mwengine wa maandamno mjini Tehran na kwengineko.
Katika sehemu fulani, pamoja na mji mkuu, majengo ya serikali yalishambuliwa.
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Abdolreza Rahmani-Fazli, aliwatuhumu wale wanaotumia mitandao ya jamii kuhimiza maandamano, kwamba wanajaribu kusambaza hofu na ghasia.
Baada ya wandamanaji wawili kuuwawa katika mji wa Dorud , wakuu wa huko walikanusha kuwa askari wa usalama walifyatua risasi.
Wamesema vifo hivyo vilitokana na wachochezi wanaowakilisha nchi za nje, na wachochezi wengine kati ya raia.
Post a Comment