0
Ni mara ya kwanza Barcelona imeweza kushinda mechi tatu za ugenini mfululizo katika uwanja wa Bernabeu, na matokeo hayo yanakiwacha kikosi cha Zinedine Zidane katika nafasi ya nne.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionNi mara ya kwanza Barcelona imeweza kushinda mechi tatu za ugenini mfululizo katika uwanja wa Bernabeu, na matokeo hayo yanakiwacha kikosi cha Zinedine Zidane katika nafasi ya nne.
Barcelona ilionyesha mchezo mzuri ugenini na kupata ushindi dhidi ya Real Madrid ambayo imeondolewa katika kuwania taji la ligi ya Uhispania.
Shambulio la kipindi cha pili la Luis Suarez na penalti ya Lionel Messi baada ya Dani Carvajal kupewa kadi nyekundu kwa kunawa mpira, bao lililosaidia Barcelona kupanda juu ya jedwali kwa alama 14 dhidi ya Real.
Karim Benzema alipiga mwamba wa goli na kukosa nafasi mbili za wazi katika kipindi cha kwanza , lakini timu hiyo ya nyumbani ilibaki bila jibu katika mechi hiyo ya El Clasico.
Los Blancos ilianza huku Gareth Bale akiwa benchi, na ijapokuwa alimlazimu kipa Marc-Andre ter Stegen kuokoa mipira baada ya kuingizwa kufuatia kutolewa kwa Carvajal, mshambuliaji huyo wa Wales alishindwa kuokoa timu yake.
Badala yake mchezaji wa ziada Aleix Vidal aliongeza chumvi katika kidonda katika dakika za lala salama kwa kupata bao la tatu.
Ni mara ya kwanza Barcelona imeweza kushinda mechi tatu za ugenini mfululizo katika uwanja wa Bernabeu, na matokeo hayo yanakiwacha kikosi cha Zinedine Zidane katika nafasi ya nne.

Post a Comment

 
Top