George Kitalama enzi za uhai wake
***
Habari zilizotufikia hivip punde zinasema kuwa kada wa Chadema Mhe.George Kitalama amefariki dunia ghafla mjini Shinyanga jioni hii Jumapili Oktoba 8,2017.
Mhe Kitalama aliwahi kuwa Diwani Kata ya Kitangiri katika manispaa ya Shinyanga kwa tiketi ya CHADEMA 2010 -2015,lakini pia amewahi kuwa Katibu CHADEMA Wilaya Shinyanga Mjini.
Inaelezwa kuwa amekutwa na umauti baada ya kuanguka akiwa kwenye kikao cha kanisa la KKKT Mjini Shinyanga.
Taarifa zaidi tutawaletea hivi punde.
R.I.P Kitalama
Post a Comment