0

Shirika la  viwanda  vidogovidogo  SIDO kwa  Kushirikiana  na  Ofisi  ya  mkuu  wa mkoa  Lindi  linatarajia kufanya Maonesho ya  biashara   kwa kukutanisha  wajasirimali zaidi 3000 wa  mikoa  ya  Lindi, Mtwara, Morogoro , Pwani  na  Ruvuma. 

Akizungumzia  tukio  hilo Kaimu  Meneja wa  Sido  Lindi  Salma Ally alisema maonesho  haya  yanatarajia  kuanza tarehe  6  Novemba  hadi  tarehe 12 Novemba 2017  yakiwa  na  lengo la kukutanisha  wajasiriamali , ili kubadilishana  uzoefu na mbinu  za kibiashara na  elimu  ya  mikopo.

Salma  Aliongeza  kwenye  maonesho hayo taasisi  mbalimbali  za umma zitatoa  elimu  kwa  wajasiriamali namna ya kutumia  frusa  za  mikopo, elimu  na teknolojia  mbalimbali.

Aidha  amewataka  wananchi  mkoani Lindi  kuungana  na  wajasiriamali wengine  kushiriki  maonesho  hayo  ili kujifunza  na  kutumia  frusa  mbalimbali zitakazo tolewa  ikiwemo elimu  ambayo itawasaidia  kuimarisha  ushindani  wa soko   na  kuwaleta pamoja  wajasiriamali wadogo, wakubwa na wale wanaochipukia ili kupata fursa ya kuuza, kuonesha na kujadili masuala ya biashara kwa ujumla.

Aliongeza  kuwa SIDO  inalenga kusaidiana na serikali katika kutimiza malengo ya milenia likiwemo  kuondoa umasikini, na kutoa  frusa  kwa  wajasiriamali  kuonesha na kuuza bidhaa zao 

Post a Comment

 
Top