0
Ndege za kijeshi za Korea Kaskazini zapaa karibu na anga ya pwani ya Korea Kaskazini kuonyesha ubabe
Image captionNdege za kijeshi za Korea Kaskazini zapaa karibu na anga ya pwani ya Korea Kaskazini kuonyesha ubabe
Ndege za kijeshi za Marekani zimepaa karibu na pwani ya mashariki ya Korea Kaskazini katika kuonyesha ubabe wa kivita, idara ya ulinzi nchini Marekani pentagon imesema.
''Hatua hiyo ni kuonyesha kuwa rais Trump ana njia tofauti za kijeshi kushinda vitisho vyovyote'' , msemaji Dana White alisema.
Marekani na Korea Kaskazini zimerushiana cheche za maneneo katika kipindi cha hivi majuzi.
Katika Umoja wa mataifa siku ya Jumanne, bwana Trump alisema kuwa ataiangamiza Korea Kaskazini iwapo Marekani italazimika kujitetea na washirika wake.
''Hili ni eneo ambalo jeshi lolote halifai kupitia na ni ndege za kijeshi za Marekani ambazo zimeweza kulifikia katika karne ya 21, licha ya tabia mbaya ya Korea Kaskazini'', alisema Bi White.
Tangazo hili lilijiri muda mfupi kabla ya waziri wa kigeni wa Korea Kaskazini kutoa hotuba yake katika umoja wa mataifa .
Mapema siku ya Jumamosi , tetemeko lenye ukubwa wa 3.4 katika vipimo vya Ritcher lilisikika karibu na kituo cha kujaribia makombora cha Korea Kaskazini na kuzua hofu kwamba taifa hilo huenda lilitekeleza jaribio jingine la kombora lake.
Lakini wataalam wamesema kuwa lilikuwa tetemeko la ardhi.

Post a Comment

 
Top