0

0 


  SAUTI YA  KUSINI.COM
Mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi,Christopher Ngubiagai ameziomba   taasisi za fedha zinazotoa mikopo kupunguza   masharti na  viwango vya riba za  mikopo

Ngubiagai anaetambulika kwa jina la Komredi alitoa wito huo wakati anafungua semina ya wajasiriamali iliyofanyika leo katika mamlaka ya mji mdogo wa Kilwa Masoko.Semina ambayo iliandaliwa na mamlaka ya mapato nchini (TRA) mkoa wa Lindi.

Alisema tasisi za fedha zinanafasi na uwezo mkubwa wakuisaidia serikali katika mkakati wake wa kuwainua wananchi wake wenye vipato vidogo ili waweze kushiriki kikamilifu ujenzi wa uchumi wa nchi kwa kulegeza baadhi ya masharti na viwango vya riba.

Mkuu huyo wa wilaya huku akionesha kuhuzunishwa na kuguswa na changamoto wanazokutananazo wajasiriamali,alisema kutokana na masharti magumu na viwango vya riba vilivyopo kwenye baadhi ya benki zinasababisha wakopaji kukosa amani na kuishi kwa hofu badala ya kufurahia mikopo wanayokopeshwa.

"Zipo taasisi na benki chache ambazo siwezi kuzitaja,zinamasharti na riba nafuu.Lakini ziponyingine ambazo pia sitazitaja,ukikopa unakosa amani,unakosa furaha na unakonda kama unanyonywa damu na jini.Siwezi kuziagiza zilege masharti na riba bali ziwahurumie wenyevipato vidogo," Komredi Ngubiagai aliomba na kusisitiza kwa njia ya utani.

Kuhusu azima ya kuvitafutia mikopo vikundi vya ujasiriamali,mkuu huyo wa wilaya alisema kwanafasi yake atahakikisha vinapata mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha zenye masharti na riba nafuu.Huku akiwahakikishia wajasiriamali hao kwamba taasisi hizo zipo na ameanza kufanyanazo mazungumzo kuhusu hilo.

Mbali na hayo,alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kupokea na kuyafanyia kazi mabadiliko,badala ya kusubiri madiliko yawabadidishe.Ikiwemo kuwa na malengo mahususi katika shuguli zao.

" Katika dunia ya leo huwezi kufanya shuguli yoyote bila elimu ukatarajia mafanikio.Hata hivyo sekta isiyorasimi inamchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi yoyote duniani,hakuna serikali iliyoweza kuwaajiri wananchi wake wote.Nawaagiza maofisa maendeleo wapeni mafunzo," alisema.

Kwa upande wake ofisa wa TRA wa kitengo cha elimu kwa walipa kodi wa mkoa wa Lindi,Odupoi Papaa,licha ya kueleza mikakati ya serikali ya kuwainua wafanyabiashara wadogo.Ikiwamo kuzifanyia marekebisho baadhi ya sheria za kodi.

Aliwaasa wafanyabiashara na wananchi kwa jumla kupeleka malalamiko na ushauri kwenye ofisi zacmamlaka hiyo ili yafanyiwe kazi. 

Post a Comment

 
Top