0


Katika kuelekea maadhimisho ya siku ya sheria Zanzibar wananchi wametakiwa kutii sheria bila ya shuruti ili kuepusha kukwazana na serikali kwa kuvunja sheria.
          


Wito huo umetolewa na Kamanda wa Jeshi la polisi wa mkoa wa mjini magharibi Hassani Nassir alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake madema mjini Unguja .
Kamanda Nasir amesema lengo la kuadhimisha siku ya sheria Zanzibar  ni kuwapa elimu wananchi juu kufanya vitendo kwa kufata sheria  ya nchi .
Aidha amewahakikishia wananchi na jamii kwa ujumla kutunza usalama wa raia na mali zao siku ya maadhimisho tarehe 9 mwezi 2 mwaka huu .
Hata hivyo amewataka wananchi kujishughulisha na harakati zao za maisha kwa kuzingatia sheria na yoyote atakae bainika kwenda kinyume na sheria ya nchi hatua kali za kisheria zitachukuliwa.
Kauli mbiu ya siku ya sheria ya mwaka huu ni simamia sheria na maadili katika utendaji haki.

Post a Comment

 
Top