0


Vijana wanaoishi Visiwani Zanzibar wameshauriwa kutumia mfumo mpya wa kuomba ajira kupitia mfumo wa kielektroniki ili kuepuka usumbufu wanapotumia njia ya kawaida.
                         


          Rai hiyo imetolewa na mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini ofisi ya rais sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma Zanzibar, Riziki Abrahaman alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa chuo kikuu cha SUMAITI Chukwani wilaya ya magharibi B Unguja.
Amesema serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupitia sekreterieti ya ajira katika utumishi wa umma imeanzisha mfumo mpya wa kuomba ajira kupitia mtandao wa e-aplication ili kuwarahisisha waombaji wa ajira kuweza kutuma maombi yao kwa haraka na bila ya usumbufu.
Ameongeza kuwa mfumo huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kuondosha kadhia kadhaa katika mchakato wa kuajiri watu kama vile rushwa  na upotevu wa nyaraka muhimu za waombaji vikiwemo vyeti vya kuzaliwa, kumaliza skuli na vyuo
 
Aidha ameawataka wanafunzi na wananchi wa Zan zibar kutumia fursa waliyonayo  kisheria ya kuomba ajira zinazotolewa na Serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania katika taasisi mbali mbali ili kunufaika na haki zao kikatiba.

Post a Comment

 
Top