Ofisi ya
mufti Zanzibar imemsimamisha ustadhi Hakim Mbarouk Hamadi wa Madrasatul
Ghinayatuli Qurani kujihusisha na masuala ya kufundisha kufuatia kitendo cha
kuwadhalilisha kwa kuwaadhibu kupita kiasi wanafunzi 11 wa madrasa yake.
Taarifa iliyotolewa kwa
vyombo vya habari na katibu wa mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga imeeleza
Hatua hiyo imekuja baada ya mazungumzo na mtuhumiwa huyo yaliyofanyika katika
kituo cha polisi cha bububu wilaya ya Magharib A unguja ambapo mwalimu huyo
anashikiliwa.
Mwalimu huyo anatuhumiwa kuwapiga wanafunzi kwa viboko kisha kuwavua nguo
katia hatua nyengine Shehe Soraga amesema mwalimu huyo
amekiri kufanya kitendo hicho lakini si kwa kiwango kinachozungumzwa.
Pamoja na hayo Afisi ya
mufti Zanzibar imelaani vikali kitendo cha mwalimu huyo wa madrasa na kuwataka
walimu wengine wa madrasa zote za unguja na pemba waache vitendo vyote vya
unyanyasaji na udhalilishaji kwa watoto vikiwemo ulawiti ,upigaji bakora kupita
kiasi pamoja na ubakaji.
Katika
hatua nyengine Jumuiya ya maimamu Zanzibar JUMAZA na wao wamelaani tukio hilo
ambapo Naibu mtendaji wa jumuiya hiyo Khamis Yussufu kulinagana na mafundisho
ya dini ya kiislamu, kuwanasihi watoto kuipenda na kuielewa dini yao.

Post a Comment