0


Masheha wa Shehia mbali mbali Zanzibar wametakiwa kufatilia na kupambana na matumizi ya misumeno ya moto ambayo imepigwa marufuku na serikali. 

Hayo yamesemwa na katibu mkuu wa wizara ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi Ali Juma Ali alipokuwa akizungumza na wadau mbali mbali wakiwemo masheha na wakuu wa wilaya amesema misumeno ya moto kwa Sasa imepigwa marufuku na haitakiwi kutumika kwa sababu imebainika kuathiri vibaya mazingira.
Hata hivyo amesema serikali inawakumbusha watendaji wa shehia wakiwemo masheha na wakuu wa wilaya kwamba misumeno hiyo haitakiwi kutumika kwa ajili ya ukataji wa miti ikiwemo minazi na miti mengine. 
Nao baadhi ya wamiliki wa ekari tatu zilizotolewa na serikali kwa ajili ya matumizi ya kilimo akiwemo Ali Hilka mkaazi wa kitumba na Issa Uledi mkaazi wa chuini wilaya ya kati wamelalamika kuvamiwa mashamba yao usiku na kukatiwa minazi saba.
Nae mkuu wa wilaya ya kati Mashavu Sukwa amesema wameanza kuchukua hatua kali kwa watu waliouza ekari tatu ambapo baadhi ya wakulima wamenyanganywa na kurudishwa serikalini.

Post a Comment

 
Top